Ticker

6/recent/ticker-posts

Dalili za hatari kwa mama mjamzito ni zipi



Dalili za hatari kwa mama mjamzito ni zipi

Moja ya Vitu ambavyo Wakina mama Wajawazito hupewa ELIMU wanapohudhuria kliniki kuanzia Siku ya Kwanza ni Pamoja na kufundishwa Kuhusu Dalili za hatari wakati wa Ujauzito(Danger Signs),

Ukiwa unafahamu Dalili za hatari wakati wa Ujauzito itasaidia sana Kuchukua hatua Mapema Pale unapoona Viashiria vya hatari kwenye Ujauzito wako.

Kwa hali ya Kawaida,Asilimia kubwa ya Mahudhurio ya Kliniki huwa Manne,lakini mabadiliko hutokea kulingana na hali ya Ujauzito wako,

Hivo basi,Mahudhurio ya kliniki huweza kuzidi MANNE(4) kulingana na Hali ya Ujauzito wako

MAHUDHURIO MANNE YA KLINIKI

  1. Hudhurio la Kwanza:Ujauzito ukiwa na umri wa kabla ya wiki 16, Lakini kila hospital huweza kuweka utaratibu wao wa Muda wa kuanza Hudhurio la kwanza la kliniki, Ila Protocol,Baada tu ya kuwa Mjamzito unatakiwa kuanza kliniki
  2. Hudhurio la Pili: Ujauzito ukiwa na wiki 20 mpaka 24
  3. Hudhurio la Tatu: Ujauzito ukiwa na wiki 28 mpaka 32
  4. Hudhurio la Nne: Ujauzito ukiwa na wiki 36 Mpaka 40

Ziko dalili nyingi ambazo zinaweza kumpata mama mjamzito na iwapo utaona dalili hizi ni vyema ukafika katika kituo cha kutolea huduma mapema iwezekanavyo.

Ziko jamii za watu ambazo zimekuwa zikichukulia dalili hizi kama hali ya kawaida na wengine wamekuwa wakijitibia nyumbani pasipo kujua madhara yanayoweza kutokea iwapo hatua stahiki hazitachukuliwa.

Je Dalili za Hatari ni Zipi?

1 Kuvuja damu Ukeni

2. Mwili kutetemeka au kupata convulsions/fits

3. Kupata Maumivu makali sana ya kichwa

4. Pamoja na macho kuona marue rue

5. Kuwa na Homa kali

6. Kupata maumivu makali sana ya Tumbo

7. Kuvimba sana miguu,uso Pamoja na mikono.

HIZI HAPA NI BAADHI YA DALILI ZA HATARI WAKATI WA UJAUZITO

1. Mama mjamzito Kuishiwa nguvu au kushindwa/kukosa nguvu za kutoka kitandani

2. Changamoto ya upumuaji (kuhema haraka haraka au kukosa pumzi)

3. Dalili zote za Degedege

4. Dalili zote za kifafa cha mimba kama vile;

  • mjamzito kuona marue rue
  • mjamzito kuvimba sana miguu,mikono na uso
  • mjamzito kuumwa sana na kichwa
  • presha kuwa juu sana pamoja na uwepo wa protein kwenye mkojo n.k

5. Homa kali au joto la mwili kuwa juu sana

6. Maumivu makali ya tumbo

7. Kupungua kwa kucheza kwa mtoto tumboni kusiko kwa kawaida. Au mtoto kuacha kucheza kabisa.

8.Chupa ya uzazi kupasuka kabla ya wakati yaani premature rupture of membrane

8. Maumivu makali ya kichwa na nuru hafifu

9. Kutokwa na damu ukeni

10. Kuvimba vidole, uso na miguu sana

11. Kutapika sana na kukosa hamu ya kula

N.K

Kila mama mjamzito pamoja na mwenza wake wana haki ya kupata elimu juu ya dalili hizi na iwapo wataziona basi ni vyema wakafika katika kituo cha afya ili kuokoa maisha ya mtoto tumboni pamoja na maisha ya mama mjamzito.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



Post a Comment

0 Comments