Ticker

6/recent/ticker-posts

Dalili Za Watoto Wenye Tatizo La Usonji



DALILI ZA WATOTO WENYE TATIZO LA USONJI

DALILI ZA WATOTO WENYE TATIZO LA USONJI NI PAMOJA NA;

- Mtoto kushindwa kuitika baada ya kuitwa jina lake au mtoto kuonekana kutokusikia kabsa wakati akiitwa jina lake

- Mtoto kushindwa kutazama watu usoni(eye contacts), kutokucheka,n.k

- Mtoto kutokuongea kabsa au kuchelewa sana kuongea kuliko kawaida

- Kupoteza uwezo wa kutamka maneno au sentensi ambazo mwanzoni alikuwa anaweza kutamka

- Mtoto kushindwa kabsa kuanzisha mazungumzo

- Mtoto kuongea huku akitoa sauti zisizozakawaida

- Mtoto kushindwa kuelewa maswali rahisi akiulizwa na watu

- Mtoto kufanya vitu vya kujidhuru mwenyewe kama vile; kujipiga mwenyewe,kujibamiza kichwa n.k

- Mtoto kutokutaka mwanga,kushtuka sana akiguswa au kusikia sauti yoyote

- Mtoto kutokutamka maneno ya kitoto mpaka afikishe umri wa mwaka mmoja na kuendelea

- Mtoto kutokuongea neno lolote mpaka afikishe kipindi cha umri wa miezi kumi na sita

- Mtoto kupoteza kabsa uwezo wake wa kuongea

- Mtoto kushindwa kufanya vitu mbali mbali kama kupunga mkono kwa wazazi au mtu yoyote kama ishara ya kumsalimia au kumuaga mpaka anapofikisha kipindi cha umri wa miezi kumi na mbili

- Mtoto kushindwa kuongea maneno zaidi ya mawili au sentensi ya maneno mpaka anapofikisha umri wa miezi 24

- Mtoto kuwa na tabia ya kukaa peke yake pamoja na kujitenga na watu N.k



Post a Comment

0 Comments