Ticker

6/recent/ticker-posts

Dawa nzuri ya kutoa harufu mbaya mdomoni



Dawa nzuri ya kutoa harufu mbaya mdomoni

Shida hii ya kutoa harufu mbaya kinywani huwasumbua watu wengi, na wengine hushtuka baada ya kuambiwa kwamba Wakati wanaongea kuna harufu mbaya inatoka mdomoni,

Katika makala hii tumechambua zaidi kuhusu chanzo cha tatizo la kutoa harufu mbaya mdomoni pamoja na Dawa nzuri ya kutoa harufu mbaya mdomoni.

Chanzo cha tatizo la kutoa harufu mbaya mdomoni

Tatizo hili husababishwa na nini? zipo sababu mbali mbali ambazo huchangia kinywa kutoa harufu mbaya,

BAADHI YA SABABU HIZO NI PAMOJA NA;

- Baadhi ya vyakula, baada ya chakula kuvunjwa vunjwa na baadhi ya mabaki ya chakula kuganda kuzunguka meno huweza kupelekea mashambulizi ya bacteria pamoja na kinywa kuanza kutoa harufu mbaya,

Kula VITUNGUU MAJI, vitunguu saumu(garlic) au viungo vingine huweza kuongeza harufu mdomoni

- Uvutaji wa Sigara ikiwemo Tumbaku, mbali na kuwa kwenye hatari ya kupata magonjwa ya fizi(gum disease) na meno,wavutaji wa sigara ikiwemo tumbuku wapo kwenye hatari ya kupata shida ya kutoa harufu mbaya mdomoni

- kUtokusafisha kinywa vizuri(Poor oral and dental hygiene), Hii ni miongoni mwa sababu kubwa ambazo hupekea kutoa harufu mbaya kinywani,

Mbali na kutoa harufu mbaya kinywani, kutokusafisha meno na kinywa vizuri hupelekea mabaki ya chakula kuganda kwenye meno, hali ambayo hupelekea watu wengi sana kuwa na matatizo ya Meno.

KUMBUKA; Wataalam wa meno na kinywa wanasema,miongoni mwa sababu kubwa za matatizo ya meno kwa wagonjwa wengi ambao wanawapata, ni kuganda kwa uchafu kwenye meno kutokana na meno kutokusafishwa vizuri.

- Shida ya mdomo kuwa mkavu(Dry mouth), Mate husaidia sana kusafisha mdomo na kuondoa mabaki ya chakula(Food particles) ambayo huweza kusababisha harufu mbaya mdomoni,

Tatizo hili la mdomo kuwa mkavu yaani Dry mouth or xerostomia huweza kusababisha harufu mbaya kutoka kinywani kwa sababu ya upungufu mkubwa wa mate mdomoni,

Hali hii ya mdomo kuwa mkavu mara nyingi hutokea usiku ukiwa umelala, ndyo maana ukiamka asubuh mdomo hutoa harufu zaidi, mbali na kuwa na mabaki ya chakula mdomoni na kwenye meno kama hukupiga mswaki.

Endapo shida hii ya mdomo kuwa mkavu(xerostomia) hutokea wakati wote bila kuondoka,inabidi upate matibabu ya tatizo hili.

- Matumizi ya dawa, baadhi ya dawa huweza kuchangia tatizo hili la kutoa haruf u mbaya kinywani kwa kukausha mdomo(dry mouth) au kwa kutoa chemicals baada ya uvunjwaji wake,ambazo huweza kuongeza harufu mdomoni.

- Maambukizi ya magonjwa kwenye meno,Fizi na kinywa, kuwa na shida ya fangasi mdomoni, maambukizi ya bacteria, kidonda baada ya kutoa jino au meno,meno kuoza,vidonda mdomoni,n.k vyote hivi huweza kusababisha tatizo la kutoa harufu mbaya mdomoni.

matatizo mengine kama vile; Kansa au saratani, metabolic disorders,(gastroesophageal reflux disease, or GERD),N.k, vyote hivi huweza kuchangia uwepo wa tatizo hili.

Dawa nzuri ya kutoa harufu mbaya mdomoni

MATIBABU YA TATIZO HILI LA KUTOA HARUFU MBAYA KINYWANI

Baada ya kufanyiwa uchunguzi wa kina pamoja na Vipimo,kisha wataalam wa afya kujua chanzo chake,ndipo tiba sahihi ya tatizo lako hufanyika.

Kama nilivyokwisha kueleza hapo juu baadhi ya sababu za tatizo hili, na matibabu yake yatahusu vyanzo vyake.

- Epuka uvutaji wa sigara ikiwemo tumbaku,

- Epuka matumizi ya Pombe,Ugoro n.k

- Hakikisha unasafisha kinywa na meno vizuri hasa baada ya kula

- Tumia mouth wash kama vile hydrogen perioxide n.k

- Epuka kutafuna vitunguu maji,vitunguu saumu,kula viungo vingi n.k

- Hakikisha unakunywa maji ya kutosha

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

 



Post a Comment

0 Comments