Ticker

6/recent/ticker-posts

Faida Za Juice Ya Miwa Mwilini



FAIDA ZA JUICE YA MIWA MWILINI

Kuna maneno mengi huongelewa mtaani hasa baada ya baadhi ya watu wakionekana kutumia juice ya Miwa hadharani,

Wengine wakisema,Kama ni Mwanaume anakunywa juice ya Miwa basi hana Nguvu za kiume hivo anajaribu kuziongeza,

Na kama ni mwanamke,basi hana Nguvu za kike na yeye pia hujaribu kuziongeza(hapa najua baadhi watashangaa maana hawajui kwamba kuna Nguvu za kike pia)

JE FAIDA ZA JUICE YA MIWA NI ZIPI?

Miwa ina faida nyingi kiafya. Juisi ya miwa inafahamika na wataalamu wa afya kwa kuwa na uwezo wa kuupa mwili nguvu kwa sababu ya ‘glucose’ iliyopo.

Kijiko kimoja cha juisi ya miwa, kina kalori 11. Madini halisi na vitamin zinazopatikana katika sukari ni kama phosphorus, calcium, madini ya chuma na potassium.

Si hivyo tu, miwa ni jamii ya tunda lenye alkali hivyo lina uwezo wa kupambana na saratani hasa ile ya kibofu cha mkojo na saratani ya maziwa.
Miwa ina upekee wake kwani ina uwezo wa kuongeza maji mwilini, inaupooza mwili na kuupa nguvu.

Virutubisho vilivyopo katika miwa vina manufaa makubwa katika kusaidia utendaji kazi wa ogani muhimu kama figo, moyo, ubongo na viungo vya uzazi.
Pia, wagonjwa wa kisukari wasihofie sukari iliyopo kwenye miwa kwani haina madhara yoyote kwao. Uzuri wa juisi ya miwa ni kuwa sukari yake ni halisia.​

USHAURI: Hivo miongoni mwa juice ambazo unashauriwa kuzitumia mara kwa mara ni pamoja na hii juice ya Miwa, japo zipo juice zingine nyingi ambazo zina faida sana mwilini kama vile;

• Juice ya embe

• Juice ya parachichi

• Juice ya Tango N.k

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.





Post a Comment

0 Comments