Ticker

6/recent/ticker-posts

IDADI YA MAYAI KWA MWANAMKE(Toka kuzaliwa kwake hadi ukomo wa Hedhi)



 IDADI YA MAYAI KWA MWANAMKE(Toka kuzaliwa kwake hadi ukomo wa Hedhi)

Je Mwanamke ana Idadi ya Mayai Mangapi toka anazaliwa mpaka ukomo wake wa hedhi yaani Menopause?

IDADI YA MAYAI KWA MWANAMKE(Toka kuzaliwa kwake hadi ukomo wa Hedhi)

Kutokana na "American College of Obstetricians and Gynaecologists (ACOG), Mtoto jinsia ya kike akiwa tumboni kwa mama yake(female fetus) Ujauzito ukiwa na wiki 20 yaani 20 Weeks Gestation age anakuwa na mayai takribani Million 6-7,

Na mayai hayo huanza Kupungua mpaka kufikia Milioni 1-2 wakati anazaliwa,

Hivo basi kutokana na ACOG Mwanamke anazaliwa akiwa na Idadi ya Mayai takribani Millioni 1-2.

Na hyo ndyo Idadi kubwa ya Mayai ambayo mpaka anafariki hataifikia tena, kwani baada ya hapo mayai yataendelea kupungua siku hadi siku toka siku ya kwanza anazaliwa.

SWALI; JE KWANINI HEDHI ISIANZE TOKA SIKU YA KWANZA MTOTO WA KIKE ANAZALIWA?

- Licha ya kwamba Mwanamke anakuwa na Mayai mengi sana(Millions of eggs) kwenye vifuko vya mayai(Ovaries),Mayai hayo yanakuwa hayajakomaa mpaka kufikia kipindi cha Balehe Yaani Puberty.

Na kwa hali ya kawaida mayai ambayo hayajakomaa hayawezi kutoka kwenye Ovaries(hivo hakuna ovulation) na kama hakuna Ovulation, hata hedhi pia haitakuwepo.

Na kipindi cha balehe huanza wakati eneo la Ubongo ambalo hujulikana kama hypothalamus kufanya kazi kubwa ya uzalishaji wa vichocheo au hormones ambayo hujulikana kama gonadotropin-releasing hormone (GnRH).

Na kwa Idadi kubwa ya Wanawake kipindi cha balehe huweza kuanza kati ya miaka 12-13 japo kuna baadhi huwahi zaidi kama miaka 8 n.k na wengine huweza kuchelewa zaidi.

Na mpaka Mwanamke kufikia kipindi cha balehe(puberty), anakuwa na Idadi ya Mayai takribani 300,000–500,000, na mayai hayo huendelea kupungua kwa kasi kila mwezi.

Mbali na mayai ambayo hupungua au kutoka kipindi cha hedhi, pia kuna sababu zingine nyingi ambazo husababisha mayai kupungua sana.

IDADI YA MAYAI KWA MWANAMKE AKIWA NA MIAKA YA 30(30s)

Mwanamke anakuwa na uwezo mkubwa sana wa kubeba mimba(high fertility) kuanzia miaka ya 20 hapo, ambapo anakuwa na asilimia 25-30% za kubeba mimba kwa kila Mwezi.

Kutokana na ACOG, wanasema uwezo wa mwanamke kubeba Mimba hupungua sana kuanzia kwenye Miaka ya 32 ambapo atakuwa na wastani wa mayai 120,000, huku uwezo wa kubeba mimba ukiwa ni wastani wa asilimia 20% kwa kila mzunguko.

Na Mayai yataendelea kupungua sana na kwa kiasi kikubwa Mwanamke akifikia umri wa Miaka 37 ambapo atakuwa na wastani wa mayai 25,000.

Kutokana na Centers for Disease Control and Prevention (CDC) wanasema, Couples Moja(1) kati ya tano(5) ambapo Mwanamke ana umri wa Miaka 30-39 Wanapata changamoto ya kupata mtoto.

UWEZO WA KUBEBA MIMBA KWA MWANAMKE MWENYE UMRI WA KUANZIA MIAKA YA 40(40S)

Kwa mwanamke mwenye umri wa Miaka 40, uwezo wa kubeba Mimba hushuka mpaka asilimia 5%, Ingawa pia kuna wanawake wengi hubeba mimba kwenye miaka hii ya 40-44,

KIPINDI CHA UKOMO WA HEDHI(Menopause)

- Wakati Mwanamke anafikia kipindi cha ukomo wa hedhi yaani menopause,anakuwa na takribani ya Mayai chini ya 1,000,

Kadri umri unavyosogea, Mayai ambayo hayajakomaa(Immature eggs) huwa resistant kwa FSH, Na kadri mayai yaliyokomaa hupungua, ndipo Ovaries huaza kuzalisha kiwango kidogo sana cha estrogen and progesterone tofauti na hapo mwanzo.

Hali hii hupelekea ukomo wa hedhi yaani Menopause, ambapo mayai hayatolewi tena kwenye ovaries(stops ovulation).

Na sababu kama vile; Idadi ya mayai ambayo umezaliwa nayo, magonjwa ambayo umeyapata kipindi cha maisha yako, matibabu ambayo umepata ikiwemo dawa n.k huweza kusababisha utofauti wa kipindi cha ukomo wa hedhi(menopause) kati ya mwanamke mmoja na mwingine.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.




Post a Comment

0 Comments