Ticker

6/recent/ticker-posts

Kuna tofauti gani kati ya dawa za PEP na ARV



 Kuna tofauti gani kati ya dawa za PEP na ARV

PEP ni combination ya dawa ambazo unatumia 1×1 au 1×2 kwa mwezi au siku 28,

kwa Lengo la kuzuia usipate maambukizi ya Ukimwi, na unatumia ndani ya Masaa 72.

Kwa Mtu Mzima, kulingana na vituo vya Kudhibiti na Kuzuia magonjwa yaani Centers for Diseases control and Prevention(CDC),

Wanashauri Kutumia hivi PEP;

ambapo huhusisha Dawa mbili yaani tenofovir pamoja na emtricitabine kwenye Kidonge Kimoja, Pamoja na Dawa nyingine ya tatu ambayo huweza kuwa kati ya raltegravir au dolutegravir.

"The preferred PEP regimen for otherwise healthy adults and adolescents is tenofovir disoproxil fumarate (TDF) (300 mg) + emtricitibine (FTC) 200 mg) once daily PLUS raltegravir (RAL) (400 mg) twice daily or dolutegravir (DTG) (50 mg) once daily)".

TOFAUTI YA PEP NA ARV

Dawa zinazotumika kwenye PEP na ARV zinafanana, ila tofauti yake kwenye kila Kidonge ni kwenye combination yake;

Mfano;

• Kidonge Kimoja cha PEP kina Combination ya Dawa mbili ambazo ni tenofovir pamoja na emtricitabine

• Ila ARV ni combination ya Dawa Tatu kwenye Kidonge Kimoja. N.K





Post a Comment

0 Comments