Ticker

6/recent/ticker-posts

Maambukizi ya fangasi ambao husababisha Madoa meusi kwenye Miguu na Mikono



Maambukizi ya fangasi ambao husababisha Madoa meusi kwenye Miguu na Mikono(Tinea nigra)

Tinea nigra ni maambukizi ya Fangasi ambao huweza kusababisha Mtu kuwa na madoa meusi au brown kwenye miguu kwa chini,kwenye viganja vya Mikono n.k

Aina hii ya Fangasi ni adimu na Hujulikana kwa Kitaalam kama Hortaea werneckii,

ambapo hawa fangasi kwa asilimia kubwa ndyo husababisha maambukizi ya tinea nigra

Fangasi hawa wanaweza kupenya Kwenye mwili wako kupitia kidonda n.k

DALILI ZA MAAMBUKIZI YA FANGASI HAWA

- Kusababisha madoa meusi au brown Chini ya Miguu kwenye sole au kwenye viganja vya Mikono

-Madoa haya huanza kidogo kidogo hali ambayo inaweza kuwa ngumu kugundua wakati yanaanza

- Madoa miguuni au mikononi kuanza kutokea baada ya kuumia n.k

(Tazama mfano wa madoa haya kwenye picha)

CHANZO CHA MAAMBUKIZI HAYA YA TINEA NIGRA

Tinea nigra ni maambukizi ya Fangasi ambao hujulikana kama Hortaea werneckii; Cladosporium werneckii, Exophiala werneckii, au Phaeoannellomyces werneckii.

Japokuwa fangasi wengine kama Stenella araguata pia wanaweza kusababisha tinea nigra.

Jamii ya Fangasi hawa hupatikana mazingira ya Unyevu unyevu sana, kwenye mizoga,vitu vilivyoharibika,mbao/mti,udongo n.k

Na huingia kwa Mtu baada ya kupata upenyo kama wa kidonda, na Moja kwa moja kuishi kwenye eneo la mwili ambapo kuna tezi nyingi za jasho kama vile miguuni na mikononi.

MATIBABU YA MAAMBUKIZI HAYA YA TINEA NIGRA

Jamii ya dawa mbali mbali huweza kutumika,kama vile keratolytic agents mfano;
• wart cream
• salicylic acid
• Whitfield’s ointment n.k

KUMBUKA; Dawa hizi ni hatari kwa Ujauzito, hivo epuka kutumia dawa hizi ukiwa Mjamzito,ongea na wataalam wa afya Kwanza, kupata Ushauri wa kina zaidi.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.





Post a Comment

0 Comments