Ticker

6/recent/ticker-posts

Madhara Ya Kitambi Kwa Wanaume



 MADHARA YA KITAMBI KWA WANAUME

Bila shaka umewahi kusikia baadhi ya watu wakisema "kuwa na kitambi sio afya ni Ugonjwa" Kauli hii ina maana kwamba kuwa mnene pamoja na kuwa na vitambi kuna madhara mengi mwilini hivo watu wajitahidi kudhibiti vitambi.

Katika makala hii tumechambua baadhi ya athari za kuwa na vitambi kwa upande wa Wanaume,ambao ndyo kwa asilimia kubwa hupatwa na tatizo hili la kuwa na kitambi,tukiwa na maana kwamba madhara ya kitambi huweza kutofautiana kati ya jinsia moja na nyingine,lakini pia kati ya umri na umri.

MADHARA YA KUWA NA KITAMBI KWA WANAUME NI PAMOJA NA;

1. Kuathiri uzalishwaji wa hormone ya kiume ambayo hujulikana kama Testosterone

2. Kuongeza uzalishwaji wa Hormones za kike kwenye mwili wa Mwanaume

3. Baadhi ya tafiti zinaonyesha kwamba,kuwa na kitambi kwa mwanaume kunaongeza uwezekano wa mwanaume kupatwa na tatizo la Saratani ya Tezi Dume yaani Prostate Cancer

4. Kuwa na kitambi kwa Mwanaume huweza kuchangia Mwanaume kuwa na Tatizo la Kupungukiwa na Nguvu za kiume

5. Kuwa na kitambi kwa Mwanaume huweza kuchangia Mwanaume kupungukiwa na hamu ya kufanya tendo la Ndoa

6. Kuwa na kitambi kwa Mwanaume huweza kuchangia Mwanaume kuwa na maumbile madogo sana au kuwa na uume mdogo kuliko kawaida

7. Matatizo mengine ambayo huweza kutokea ni pamoja na;

• Kuwa katika hatari ya kupatwa na magonjwa mbali mbali kama vile; magonjwa ya Moyo,Presha,kisukari pamoja na magonjwa ya Figo

• kuwa katika hatari ya kupatwa na tatizo la choo kigumu yaani Constipation mara kwa mara

• Kuwa katika hatari ya kupatwa na tatizo la Bawasiri

• Kupatwa na matatizo ya kuumwa miguu mara kwa mara, maumivu ya joints,kupatwa na tatizo la miguu kuwaka moto mara kwa mara pamoja na miguu kuvimba

• Uchovu kupita kiasi hata kama umefanya kazi ndogo sana N.k

Hivo basi,Kama una kitambi unashauriwa kutumia njia mbali mbali za kupunguza kitambi ulichonacho ili kuepuka athari zake, Fanya mazoezi ya mwili kila siku angalau kwa dakika 30 au Nusu saa,epuka kula vyakula vya mafuta mengi pamoja na kutumia njia nyingine za kitaalam kwa ajili ya kupunguza uzito na vitambi.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.





Post a Comment

0 Comments