Ticker

6/recent/ticker-posts

Madhara ya nyama za puani,Soma hapa kufahamu madhara ya nyama za puani



Madhara ya nyama za puani,Soma hapa kufahamu madhara ya nyama za puani.

Kama unatatizo la nyama za puani,au una mtoto,ndugu, jamaa au rafiki, haya ndyo madhara yanaweza kutokea kwao endapo wana shida hii ya nyama za puani;

1. Kupata shida ya kupumua,kukosa hewa, kutokuvuta na kutoa hewa vizuri, pamoja na kutoa sauti au kusikika kwa sauti wakati wa kupumua

2. Kupata shida ya pua kuvimba, au kuwa na tatizo la Runny, stuffy nose,

Ingawa mara nyingi nyama hizi hazisababishi maumivu yoyote,mtu huweza kupata madhara kama haya

3. Kuwa na tatizo la mafua ambayo haishi, mafua ya mara kwa mara

4. Kuwa na shida ya unyevu unyevu au makamasi kushuka chini ya koo, tatizo ambalo kitaalam hujulikana kama postnasal drip.

5. Kutokuwa na uwezo wa kuhisi harufu ya vitu vizuri au Kutokuwa na uwezo wa kunusa.

6. Kutokuwa na uwezo wa kujua ladha ya vitu mdomoni(taste)

7. Kupata maumivu ya Uso au kichwa mara kwa mara

8. Wakati mwingine unaweza kuhisi maumivu mpaka kwenye meno

9. Mtu kuhisi hali ya kichwa kuwa kizito sana

10. Mtu Kukoroma n.k

NB: Hakikisha unawahi kwa daktari endapo nyama za puani zinakuletea dalili kama hizi;

✓ Kwanza pale ambapo dalili nilizozitaja hapo juu zinazidi kuwa mbaya

✓ Unaona marue rue,huoni vizuri au unapata mabadiliko ya uwezo wa kuona

✓ Kichwa kinavimba kwa mbele

✓ Unapata maumivu kuzunguka macho au eneo linalozunguka macho kuvimba

✓ Maumivu makali sana ya kichwa

✓ Shingo kukakamaa n.k

SOMA Zaidi Hapa: Tatizo la Nyama za Puani,Chanzo chake na Matibabu yake

AU KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

= Rejea za Mada;

  • Mayoclinic; https://www.mayoclinic.org/diseases-conditions/nasal-polyps/symptoms-causes/syc-20351888
  • afyaclass: http://cdp.pvh.mybluehost.me



Post a Comment

0 Comments