Ticker

6/recent/ticker-posts

Mbio za kuleta faraja kwa watoto waliozaliwa na tatizo la afya ya akili (Usonji)



Mbio za kuleta faraja kwa watoto waliozaliwa na tatizo la afya ya akili (Usonji)

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa leo Septemba 07, 2024 ameshiriki matembezi ya hisani ya 𝐌𝐚𝐞𝐧𝐝𝐞𝐥𝐞𝐨 𝐁𝐚𝐧𝐤 𝐌𝐚𝐫𝐚𝐭𝐡𝐨𝐧 ‘Hatua ya Faraja’ Msimu wa Pili Jijini Dar es Salaam

Mhe. Majaliwa ameongoza mbio hizo za kuleta faraja kwa watoto Lengo likiwa ni kukusanya zaidi ya milioni 200 kwa ajili ya Kuchangia ukarabati wa Kituo cha watoto waliozaliwa na tatizo la afya ya akili (Usonji) wa kituo cha Mtoni Diakonia na pia kwa ajili ya kununua mashine maalum za kuwahifadhi watoto wanaozaliwa kabla ya wakati yaani watoto njiti, katika Hospitali ya rufaa ya KCMC.

Katika mbio hizo Waziri mkuu ameambatana na Naibu waziri wa afya Dkt. Godwin Mollel pamoja na viongozi wengine wa serikali ikiwa ni kuunga mkono juhudi za kuendelea kuboresha sekta ya afya katika kutoa huduma bora kwa wananchi.





Post a Comment

0 Comments