Ticker

6/recent/ticker-posts

Mkanda wa Jeshi,chanzo,dalili na matibabu yake



Mkanda wa Jeshi,chanzo,dalili na matibabu yake

Fahamu kuhusu Mkanda wa Jeshi, maana yake,chanzo,dalili,pamoja na matibabu yake,kupitia makala hii.

Mkanda wa Jeshi

Mkanda wa Jeshi ni tatizo linalohusu maambukizi ya Virusi(Viral Infection) ambayo hutokana na reactivation ya varicella-zoster virus,

Tatizo hili la Mkanda wa Jeshi kwa jina lingine hujulikana kama Herpes zoster au Shingles.

Dalili za Mkanda wa Jeshi

Tatizo la Mkanda wa Jeshi huweza kuhusisha maumivu pamoja na uwepo wa vipele kwenye eneo flani yaani self-limited dermatomal rash,

Na mara nyingi mkanda wa jeshi huanza na maumivu kwenye eneo lililoathiriwa na virusi hawa,

ambapo huambatana na kuanza kujitokesha mabadiliko ya ngozi kwenye eneo hilo ndani ya siku 2 mpaka 3.

Mkanda wa jeshi ni jina linalotumika sana mitaani kuutaja ugonjwa unaoshambulia ngozi na kujenga tabaka la vijipele vikubwa venye majimaji ambavyo mara nyingi hukamata upande mmoja wa mwili.

Ingawa vijipele vya mkanda wa jeshi vinaweza kutokea sehemu yo yote ya mwili, mara nyingi hupenda kuota kifuani, shingoni, usoni, mgongoni na mikononi.

Vijipele hivi hukaa juu ya ngozi kwa muda wa wastani wa wiki mbili hadi sita kisha hupotea. Vipele vya mkanda wa jeshi huambatana na maumivu makali na kusikia ngozi kuwaka moto.

?KUMBUKA: SIO KILA MWENYE MKANDA WA JESHI NI MUATHIRIKA WA UKIMWI

Watu ambao wapo kwenye hatari ya Kupata Mkanda wa Jeshi

‣ Mkanda wa jeshi huwapata zaidi watu wenye umri mkubwa,

Mfano; watu wenye umri wa zaidi ya miaka 50,

utafiti unaonyesha kuwa zaidi ya nusu ya watu wenye umri wa zaidi ya miaka 80 hupatwa na mkanda wa jeshi.     

‣  Vilevile huwapata zaidi watu waliopatwa na magonjwa yanayopunguza kinga za mwili, kama vile, UKIMWI na saratani.

‣ Tiba za mionzi na chemotherapy huweza kupunguza kinga ya mwili kwa mgonjwa na kumfanya awe kwenye hatari kubwa ya kupata mkanda wa jeshi.

Matibabu ya Mkanda wa Jeshi

Matibabu ya mkanda wa Jeshi ni pamoja na matumizi ya dawa mbali mbali jamii ya antiviral medications kama vile;

  •  acyclovir,
  • famciclovir,
  • Pamoja na valacyclovir ambazo hutolewa ndani ya saa 72 toka dalili kujitokeza

FAQs: Maswali ambayo huulizwa mara kwa mara

Je,Mkanda wa Jeshi ni kiashiria kwamba una maambukizi ya Virusi vya Ukimwi?

Jamii imezoea kwamba Kila Mtu mwenye Mkanda wa Jeshi ni muathirika wa Ukimwi, ifahamike kwamba SIO KILA MWENYE MKANDA WA JESHI NI MUATHIRIKA WA VIRUSI VYA UKIMWI,

mtu yoyote huweza kupata mkanda wa jeshi(herpes zoster/shingles) au maambukizi ya Varicella-Zoster Virus.

Ingawa Mkanda wa jeshi huweza kuwapata zaidi watu waliopatwa na magonjwa yanayopunguza kinga za mwili, kama vile, UKIMWI, saratani n.k.

Hitimisho

Ni munimu kufahamu kuhusu dalili za mkanda wa jeshi,ili zikianza kujutojeza upate msaada wa haraka zaidi,

Dalili za Mkanda wa Jeshi ni pamoja na;

Mkanda wa jeshi ni jina linalotumika sana mitaani kuutaja ugonjwa unaoshambulia ngozi na kujenga tabaka la vijipele vikubwa venye majimaji ambavyo mara nyingi hukamata upande mmoja wa mwili.

Ingawa vijipele vya mkanda wa jeshi vinaweza kutokea sehemu yo yote ya mwili, mara nyingi hupenda kuota kifuani, shingoni, usoni, mgongoni na mikononi.

Vijipele hivi hukaa juu ya ngozi kwa muda wa wastani wa wiki mbili hadi sita kisha hupotea. Vipele vya mkanda wa jeshi huambatana na maumivu makali na kusikia ngozi kuwaka moto.

KWA USHAURI ZAIDI/ELIMU/TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



Post a Comment

0 Comments