Ticker

6/recent/ticker-posts

Mwanamuziki Mkongwe Sergio Mendes Afariki dunia baada ya Kuugua Uviko 19



Mwanamuziki Mkongwe Sergio Mendes Afariki dunia baada ya Kuugua Uviko 19

MWANAMUZIKI Mkongwe wa Brazil, Sergio Mendes (83), amefariki dunia jijini Los Angeles baada ya kuugua Uviko19 iliyomsumbua kwa muda mrefu.

Mpiga Piano na Mwandishi huyo wa nyimbo ni mmoja kati ya watu wa kwanza kuutambulisha Muziki wa Brazil “Genre bossa nova” Kimataifa katika miaka ya 1960 kupitia wimbo wake maarufu wa Mas Que Nada.

Mshindi huyo wa tuzo za Grammy amewahi kufanya kazi na Wanamuziki mashuhuri kama Stevie Wonder, Black Eyed Peas na Justin Timberlake.

Mwezi Novemba mwaka jana Mendes alifanya show zilizofanikiwa kuuza tiketi zote jijini Paris, London na Barcelona.



Post a Comment

0 Comments