Ticker

6/recent/ticker-posts

Tatizo la Masikio Kupoteza Usikivu,Chanzo,Dalili na Tiba yake,



Tatizo la Masikio Kupoteza Usikivu,Chanzo,Dalili na Tiba yake,

Tatizo la Kupoteza Usikivu kwa Mtu huweza kusababishwa na Sababu mbali mbali ikiwemo Uzee(Umri mkubwa) Pamoja na mtu kukaa kwenye mazingira ya makelele mengi makubwa kwa muda mrefu,

Sababu zingine kama vile masikio kuwa na Nta kupita kiasi(excessive earwax), pia huweza kupunguza usikivu wa masikio kwa Muda.

Wakati mwingine kulingana na chanzo cha tatizo hili huwa vigumu kwa masikio kurudisha usikivu wake kama Mwanzo,ila tiba ikasaidia tu kupunguza baadhi ya madhara,

Soma zaidi hapa chini....!!!!

DALILI ZA TATIZO HILI LA MASIKIO KUPOTEZA USIKIVU WAKE NI PAMOJA NA;

- Mtu kuanza kupata shida ya kuelewa maneno kutoka kwa watu wengine hasa wakiongea mazingira yenye kelele au watu wengi

- Mtu kuanza kuongea kwa Sauti kubwa sana, bila kujua anaongea kwa sauti kubwa zaidi kwa wengine

- Kuomba mara kwa mara watu wengine kuongea taratibu ila kwa Sauti kubwa ili usikie vizuri

- Kuhitaji Sauti ya TV au REDIO kuwa Juu Zaidi ili usikie vizuri

- Kuhitaji Sauti ya Simu Kuwa Juu zaidi ili uweze kusikia vizuri wakati wa mazungumzo n.k

CHANZO CHA TATIZO HILI NI NINI?

mara nyingi tatizo la Masikio kupoteza usikivu wake hutokana na;

1. kuharibiwa kwa sehemu ya ndani ya sikio(inner ear), Na hii husababishwa na sababu mbali mbali kama vile; Uzee(umri mkubwa), mtu kukaa kwenye mazingira yenye makelele mengi makubwa kwa muda mrefu n.k,

Vitu hivi huweza kusababisha shida kwenye vinyweleo au Nerve cells kwenye eneo la cochlea,

Kumbuka vinyweleo hivi au Nerve cells hizi ndyo hutuma taarifa(sound signals) kwenda kwenye Ubongo, Hivo baada ya kuharibiwa haziwezi tena kufanya kazi vizuri hivo tatizo la upotevu wa usikivu hutokea.

2. Kujengwa kwa Nta taratibu ndani ya sikio(Earwax), Nta ikizidi huweza kuziba ear canal na kuzuia upitishwaji wa Mawimbi ya Sauti,

Hivo kuondoa uchafu huu(Nta/earwax) huweza kurudisha usikivu wa sikio lako.

3. Maambukizi ya Sikio, masikio kushambuliwa na vimelea mbali mbali vya magonjwa kama bacteria,fangasi,virusi n.k huweza kuleta tatizo la masikio kupoteza usikivu wake

4. Kuwa na shida ya kimaumbile kwenye mfupa eneo la sikio(abnormal bone growths), hii hutokea tangu ukiwa tumboni

5. Uwepo wa tatizo la Uvimbe ndani ya sikio, hasa sehemu ya nje au katikati ya sikio(outer or middle ear),

Hii pia huweza kusababisha masikio kupoteza usikivu wake.

6. Kupatwa na Tatizo la Kupasuka NGOMA ya SIKIO(Ruptured eardrum),

Makelele mengi,Sauti kubwa sana, mabadilikio ya gafla ya Presha,kuingiza kitu chenye ncha kali sikioni,maambukizi ya magonjwa n.k,

Vyote hivi huweza kusababisha tatizo la Ngoma ya Sikio kupasuka,kisha Mtu kupoteza Usikivu wake. N.K

VITU HIVI HUONGEZA HATARI YA KUPATA TATIZO LA KUPOTEZA USIKIVU MASIKIONI

- kuwa na Umri Mkubwa(Uzee)

- Kufanya kazi kwenye mazingira yenye makelele mengi na makubwa mara kwa mara,

Au kukaa kwenye mazingira yenye makelele zaidi kila mara,makelele ya mziki mkubwa, makelele ya milipuko mikubwa ya mabomu,vyuma kugongwa sana n.k

- Kuwa na Mtu mwenye tatizo hili ndani ya Familia yako(heredity)

- Matumizi ya baadhi ya Dawa hovio pasipo maelekezo ya kina kutoka kwa wataalam wa afya,mfano dawa kama; gentamicin, sildenafil (Viagra) au dawa jamii ya chemotherapy drugs, huweza kuharibu sehemu ya ndani ya sikio(inner ear).

Kutumia Dose kubwa za aspirin au dawa zingine za maumivu(pain relievers), Dawa za Malaria(antimalarial drugs) N.k

- Kupatwa na magonjwa ambayo husababisha Homa kali(high fever), kama vile meningitis n.k, huweza kuharibu eneo la cochlea ndani ya sikio."

MATIBABU YA TATIZO HILI LA KUPOTEZA USIKIVU

Zipo tiba mbali mbali kulingana na chanzo husika,ila kwa Ujumla,tiba huweza kuhusisha;

- Kuondoa uchafu au Nta zinazoziba masikio(Removing wax blockage).

- Upasuaji kwa baadhi ya matatizo

- Kutumia Dawa za kutibu infections mbali mbali

- Kutumia vifaa vya kuongeza Usikivu(Hearing aids). N.K

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



Post a Comment

0 Comments