Ticker

6/recent/ticker-posts

Tatizo la mdomo kuwa mwekundu chanzo chake na Tiba yake



 Tatizo la mdomo kuwa mwekundu chanzo chake na Tiba yake

CHANZO CHA TATIZO LA MDOMO AU LIPS ZAKE KUWA NYEKUNDU SANA

Tatizo la mdomo kwa ndani au kwenye lips kuwa na rangi nyekundu sana kuliko kawaida huweza kutokea kwa mtu yoyote, na kwa wengine hali hii huambatana na maumivu, kuhisi kuchomwa chomwa mdomoni,kuwashwa,kuvimba n.k

Maeneo ambayo huweza kuathirika na tatizo hili la wekundu usio wa kawaida ni pamoja na; mdomo(ndani),lips, ulimi pamoja na Fizi za meno.

CHANZO CHA TATIZO LA MDOMO AU LIPS ZAKE KUWA NYEKUNDU SANA

- Tatizo hili huweza kumpata mtu kutokana na sababu mbali mbali lakini sababu kubwa huweza kuwa mbili yaani;

1. Mtu kupata tatizo la kuumia mdomoni

2. Au kushambuliwa na vimelea vya magonjwa mbali mbali kama vile;

Bacteria,virusi au Fangasi ambao hushambulia ngozi nyembamba ndani mdomoni au kwenye lips

Hivo basi, tunaweza kusema magonjwa ambayo husababisha hali hii ni kama vile;

- Maambukizi ya virusi vya ukimwi

- Maambukizi ya virusi vya Herpes Simplex Virus

- Maambukizi ya Fangasi wa mdomoni

- Maambukizi ya fangasi wa kwenye ulimi n.k

3. Mtu kuwa na Matatizo kama leukemia pamoja na magonjwa mengine kama ya Ngozi,Saratani mdomoni n.k

4. Mtu kuwa na tatizo la Allergies au Mzio kwenye vitu mbali mbali ikiwemo vyakula,nyama,mafuta n.k

5. Upungufu wa Virutubisho mwilini kama Vile Vitamin B n.k, ambapo moja ya dalili zake ni pamoja na;

- Mdomo au Lips za mdomo kubadilika rangi na kuwa nyekundu n.k

- Mdomo kukauka Sana

- Mdomo,Lips za mdomo au Ulimi kupasuka n.k

DALILI AMBAZO MTU MWENYE TATIZO HILI HUWEZA KUZIPATA

• Joto la mwili kuwa juu au mgonjwa kuwa na homa

• Mgonjwa kupata uchovu wa mwili usio wa kawaida

• Mdomo wa mgonjwa kukauka sana kuliko kawaida

• Mgonjwa kukosa kabsa hamu ya kula chakula

• Mgonjwa kuhisi hali ya kuchomwa chomwa au kuungua moto mdomoni

• Mgonjwa kuanza kupata vipele au vidonda mdomoni

• Na kwa wengine mdomo huanza kuvimba wenyewe

MATIBABU YA TATIZO HILI

- Mgonjwa ataanza kupata matibabu kulingana na chanzo chake, mfano kama ni maambukizi ya fangasi wa mdomoni, mgonjwa ataanza kutibiwa fangasi, Kama ni maambukizi ya bacteria basi tipa itahusu eneo hili n.k

Hivo mgonjwa lazima aende hospital kwanza,kwa ajili ya uchunguzi wa kina ikiwa ni pamoja na vipimo na Tiba.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.





Post a Comment

0 Comments