Ticker

6/recent/ticker-posts

Tatizo la SIKIO AU MASIKIO KUZIBA,chanzo,Dalili na Tiba



 Tatizo la SIKIO AU MASIKIO KUZIBA,chanzo,Dalili na Tiba

• • • • • •

FAHAMU KWA KINA TATIZO LA KUZIBA KWA SIKIO KUTOKANA NA NTA PAMOJA NA CHANZO CHAKE

Moja ya vyanzo vikubwa vya tatizo la kuziba kwa sikio ni NTA. Maana ya NTA, Hapa tunazungumzia kuhusu vitu vyenye asili ya umaji umaji pamoja na mnato ambavyo hupatikana ndani ya sikio.

Kazi ya NTA sikioni ni pamoja na Ulinzi wa sikio juu ya vitu vinavyoingia,ambapo NTA huweza kunata, kushikilia pamoja na kuzuia kitu kisipite ndani ya sikio Kwa haraka,Mfano wale wadudu wadogo wadogo ambao hupenda kuingia ndani ya sikio huweza kunaswa hapa. Lakini pia nta husaidia katika kusafisha sikio, pamoja na kulainisha Sikio.

SABABU ZA NTA KUZIBA SIKIO NI PAMOJA NA;

- Uwepo wa Nta kupita kiasi sikioni huweza kusababisha tatizo la Sikio kuziba, Lakini hali hii huweza kusababishwa na vitu mbalimbali ikiwemo mashambulizi ya magonjwa mbalimbali ndani ya sikio.

- Kuwa na tabia ya kupenda kutumia pamba katika kusafisha masikio, Pamba zingine huweza kunaswa na NTA hivo kupelekea hali ya Sikio kuziba

- Kutumia mara kwa mara carotenoids

-  Hali ya kimaumbile ya mtu ambapo mtu huzaliwa na udhaifu flani ndani ya sikio

DALILI ZA TATIZO LA SIKIO KUZIBA KUTOKANA NA NTA NI PAMOJA NA;

1. Kuanza kupata hali ya kukohoa mara kwa mara

2. Kuanza kutoa harufu mbaya sikioni

3. Kuwa na maumivu ya sikio

4. Sikio kuanza kutoa Uchafu

5. Kupata hali ya muwasho ndani ya Sikio

6. Kuhisi hali ya uzito wa sikio

7. Kusikia kelele kama za kengele masikioni

8. Sikio kupoteza uwezo wake wa Kusikia

MADHARA YA KUZIBA KWA SIKIO KUTOKANAKO NA NTA.

1. Sikio kupoteza uwezo wake wa kusikia

2. Miwasho ya mara kwa mara sikioni hasa hasa kwenye Mlango wa kuingilia Ndani

3. Kero ya kusikia kengele masikioni kila mara

4. Ngoma ya sikio kupatwa na hatari ya kutoboka

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.





Post a Comment

0 Comments