Ticker

6/recent/ticker-posts

Ugonjwa wa Sinonasal carcinoma,Chanzo,dalili,Tiba



Ugonjwa wa Sinonasal carcinoma,Chanzo,dalili,Tiba

Hii ni aina ya Saratani adimu kutokea na huathiri zaidi eneo la puani-nasal cavity au paranasal sinuses,

Aina hii ya Saratani(Kansa) huweza kumpata Mtu yoyote, kwenye eneo Lolote duniani,bila kujali jinsia yake wala umri wake,

Japo Inaonekana kuna uwezekano mkubwa kwa wanaume kuliko wanawake kupata ugonjwa huu.

DALILI ZA SINONASAL CARCINOMA

Dalili za Mwanzoni kabsa za Saratani hii ni Pamoja na;

- Mtu kutoa damu puani

- Mtu kupata maumivu ya Uso,

- Uso kuwa na ganzi,kuchoma choma n.k

- Pua kuvimba,maarufu kama Runny Nose

- Kuona marue rue,

- Kupata maumivu ya kichwa

- Kuwa na tatizo la Pua kuziba(Nasal obstruction)

- Uwepo wa Vivimbe(tumors) n.k

Vivimbe hivi kwa kawaida hutambuliwa kwa kutumia kipimo cha MRI au CT Scan ya ubongo na paranasal sinuses.

CHANZO CHA TATIZO HILI,

Hakuna Sababu ya Moja kwa moja ambayo inajulikana kama chanzo halisi cha tatizo hili, ila zipo baadhi ya Sababu zimeonekana kuwa na uhusiano wa karibu na tatizo hili,na Sababu hizo ni kama vile;

• Uvutaji wa sigara

• Mtu kuwa kwenye mazingira yenye Carcinogens,kama vile kwenye machimbo ya madini,

migodi ya makaa ya mawe na viwanda vya plating vya chrome,

wafanyakazi wa kusafisha nikeli n.k

Japo pia utafiti uliofanyika nchini Canada kwenye kiwanda Kimoja cha NIKELI,ulionyesha hata ambao sio wafanyakazi kwenye eneo la kusafishia Nikeli bado waliumwa na aina hii ya Saratani, Hivo bado chanzo halisi hakijulikani ni nini.

MATIBABU YA TATIZO HILI NI YAPI?

Zipo tiba mbali mbali kulingana na hatua ya Ugonjwa,Pamoja na Hali ya Mgonjwa,ikiwemo;

✓ Huduma ya UPASUAJI

✓ Huduma ya Mionzi(radiotherapy)

✓ Huduma ya chemotherapy kwa baadhi ya Cases n.k

#Saratani:MAGONJWA

#VIa:Afyaclass



Post a Comment

0 Comments