Ticker

6/recent/ticker-posts

Umuhimu Wa Kumfanyia Mtoto Massage



 UMUHIMU WA KUMFANYIA MTOTO MASSAGE

Unaweza ukashangaa kwamba hivi hii nayo inafaida kwa mtoto,

Ila ukweli ni kwamba kumfanyia mtoto massage ya mwili mara kwa mara kuna faida,

Faida hizo ni pamoja na;

- Kumsaidia mtoto apate choo vizuri,hapa nazungumzia massage inayohusisha tumbo,

ambapo watoto wengi wenye shida ya tumbo kuuma,kujaa gesi na kukosa choo, huanza kupata choo tena kingi baada tu ya kufanyiwa massage ya vitumbo vyao

- Massage ya mwili humsaidia mtoto kupata joto la mwili ambalo ni muhimu sana kwake,

- Massage huweza kusaidia kupunguza maumivu wakati wa meno ya mtoto kuota

- Massage huboresha afya ya misuli pamoja na viungo vya mtoto

- Massage humsaidia mtoto kutulia hata kama alikuwa analia lia na kusumbua

- Massage huweza kumsaidia mtoto kupata usingizi mzuri zaidi. N.k

HIZO NDYO BAADHI YA FAIDA ZA MASSAGE KWA MTOTO.



Post a Comment

0 Comments