Ticker

6/recent/ticker-posts

Upungufu wa nguvu za kiume,chanzo,Dalili na Tiba yake



Upungufu wa nguvu za kiume,chanzo,Dalili na Tiba yake

TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME,CHANZO,DALILI NA TIBA

Tatizo la upungufu wa nguvu za kiume huweza kuhusisha; Uume kushindwa kabsa kusimama, uume kutokusimama kwa muda mrefu, Kukosa nguvu ya kuanza au kuendelea na tendo n.k

hali ambazo hupelekea mwanaume kushindwa kumridhisha mwenza wake ambaye anashiriki naye tendo la ndoa kwa wakati huo.

CHANZO CHA TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME

Zipo sababu nyingi sana ambazo huchangia wanaume kuwa na tatizo hili la Kukosa nguvu za kiume, na baadhi ya sababu hizo ni pamoja na;

- Mtindo mzima wa maisha kwa mwanaume ikiwemo ulaji wake wa kila siku

- Mwanaume kuwa na magonjwa ya moyo ambayo huweza kuathiri usafirishaji wa damu mwilini

- Uwepo wa kiwango kikubwa cha lehemu yaani High cholesterol unaweza kusababisha tatizo la uume kushindwa kusimama vizuri(erectile dysfunction)

- Tatizo la kuwa na kiwango kidogo cha hormones za kiume yaani Low testosterone Level

- Tatizo la Clogged blood vessels (atherosclerosis)

- Ugonjwa wa presha ya kupanda yaani High blood pressure huweza kuleta effect mpaka kwenye mfumo wa uzazi

- Ugonjwa wa kisukari(Diabetes),huweza kuathiri uwezo wa mwanaume kufanya tendo la ndoa ikiwemo tatizo hili la uume kushindwa kusimama vizuri yaani erectile dysfunction

- Tatizo la Uzito kuwa mkubwa yaani Overweight/Obesity, Mwanaume mwenye uzito mkubwa sana,Bonge n.k anaweza kushindwa kufanya vizuri hata kwenye tendo la ndoa.

Hivo unashauriwa kuhakikisha unazuia tatizo hili la uzito kuwa mkubwa/kupita kiasi.

- Tatizo la Metabolic syndrome, ambalo huhisisha vitu hivi kwa ujumla wake; Presha kuwa kubwa zaidi,Level ya Insulin kuwa kubwa sana,Mafuta ya mwili(Body fat) kuzidi pamoja na kiwango cha cholestrol kuwa kikubwa zaidi.

- Matatizo mengine kama vile;Parkinson's disease,Multiple sclerosis n.k pia huweza kuleta athari kwenye mfumo wa uzazi

- Uvutaji wa Sigara ikiwemo matumizi ya Tumbaku(Tobacco)

- Matumizi ya baadhi ya Dawa kama vile dawa jamii ya antidepressants, antihistamines,dawa za kutibu presha(high blood pressure), maumivu au matatizo ya tezi dume

- Unywaji wa Pombe kupita kiasi pamoja na aina nyingine za ulevi au madawa ya kulevyia

- Ugonjwa wa Peyronie's disease, ugonjwa huu huhusisha kutokea na kuendelea kwa kovu(Scar tissues) ndani ya Uume

- Tatizo la kukua kwa tezi dume(enlarged prostate),kansa/Saratani ya Tezi Dume(prostate cancer) pamoja na Matibabu yake

- Mwanaume kuumia au kupata majeraha kwenye maeneo ya via vyake vya uzazi ikiwemo kwenye nyonga pamoja na uti wa mgongo

- Mwanaume kufanyiwa upasuaji kwenye eneo la nyonga(Pelvic) au uti wa mgongo(Spinal cord)

- Tatizo la msongo wa mawazo,hofu,wasi wasi pamoja na matatizo mengine ambayo huhusisha afya ya akili(mental health problems),Vitu hivi huweza kuleta athari mpaka kwenye uwezo wako wa kufanya tendo la ndoa.

- Migogoro ya kila mara kwenye mahusiano yako ambayo pia huweza kuleta tatizo la msongo wa mawazo au stress,wasi wasi,hofu n.k

- Pia tafiti zinaonyesha kadri Mwanaume anavyokuwa na umri mkubwa(mzee) ndivo na nguvu zake za Kiume huendelea kupungua sana ikiwemo uwezo wa uume kusimama vizuri na kwa muda mrefu.

- Baadhi ya matatibu kama vile;Upasuaji wa Tezi Dume(prostate surgery) au huduma ya mionzi(radiation treatment) kwa wagonjwa wa kansa pia huweza kuathiri uwezo wa tendo kwa mwanaume

- Pamoja na Sababu zingine...

Dalili za Tatizo la Upungufu wa Nguvu za Kiume

DALILI ZA TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI PAMOJA NA;

• Uume kushindwa kusimama kabsa

• Uume kutokusimama vizuri

• Uume kusimama ila sio kwa muda mrefu

• Mwanaume kushindwa kurudia tendo, goli moja chali hawezi tena kurudia tendo

• Mwanaume kuwahi kufika kileleni na kushindwa kabsa kuendelea

• Kukosa kabsa hisia au hamu ya kufanya tendo la ndoa n.k

Madhara ya Tatizo la Upungufu wa Nguvu za Kiume

MADHARA YA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NI PAMOJA NA;

✓ Mwanaume kushindwa kumridhisha mwenza wake wakati wa tendo la ndoa

✓ Kuongeza wasi wasi,woga na hofu kubwa ya kufanya mapenzi kwa Mwanaume

✓ Mwanaume kutokujiamini tena

✓ Mwanaume kukosa kabsa hamu ya kufanya tendo la ndoa

✓ Kuanza migogoro kwenye mahusiano au ndoa,kusalitiana n.k

ERECTILE DYSFUNCTION

Shida Ya Uume Kushindwa Kusimama Na Kufanya Kazi Vizuri Wakati Wa Tendo La Ndoa.

Kutokana na Mfumo wa maisha yetu,kazi tunazofanya,vyakula tunavyokula au mtindo wa maisha kwa ujumla, tunajikuta kupata madhara mbali mbali katika miili yetu pasipo kujua sababu hasa ni ipi.

Tatizo hili la uume kushindwa kusimama na kufanya kazi vizuri,huwatokea wanaume wengi kwa hivi sasa, na kusababisha madhara makubwa yakiwemo ya mahusiano au Ndoa kuvunjika.

Chanzo cha tatizo la Erectile dysfunction

JE SABABU ZA TATIZO HILI NI ZIPI?

Zipo Sababu mbali mbali ambazo huweza kuchangia hali hii ikiwemo;

✓ Uchovu wa mwili kupita kiasi kutokana na shughuli nyingi za Siku nzima

✓ Kuwa na shida ya msongo wa mawazo au Stress huweza kusababisha hali hii

✓ Kutawaliwa na wasiwasi pamoja na hofu kubwa wakati wa tendo la Ndoa

✓ Matumizi ya dawa za kulevya pamoja na Uvutaji wa Sigara

✓ Kuwa na umri mkubwa

✓ Ukiwa unatumia baadhi ya Dawa flani

✓ Kuwa na shida ya uzito kupita kiasi au Unene huweza pia kuchangia hali hii

✓ Kuwa na historia ya kupata tatizo katika sehemu za siri siku za nyuma

✓ Kuwa magonjwa mbali mbali kama magonjwa ya moyo, presha au kisukari

✓Kujihusisha na tabia ya kufanya Punyeto au masterbution n.k

DALILI ZA TATIZO HILI LA ERECTILE DYSFUNCTION

- Hamu ya tendo la Ndoa kupote kabsa au kukosa hisia za kufanya mapenzi

- Kupata wasiwasi kabla ya kuanza kufanya mapenzi kuhusu kumridhisha mwenza wako

- Hali ya uume kusinyaa mapema

- Hali ya uume kushindwa kusimama kabsa

- Uume kunyong'onyea wakati wa tendo la ndoa n.k

TIBA YA TATIZO HILI LA ERECTILE DYSFUNCTION

Mgonjwa atatibiwa baada ya chanzo cha tatizo kujulikana hivo matibabu yake yatahusu chanzo cha tatizo lake,ambapo kwa ujumla wake, 

Mgonjwa anaweza kupewa ushauri wa kumsaidia kukaa sawa, mtindo wa maisha kuubadilisha ikiwemo vyakula,kazi n.k Pamoja na Dawa ikiwa shida hii itahitaji matibabu ya Dawa.

  • Dawa
  • Upasuaji
  • Kubadilisha Mtindo wa Maisha

Zingatia Vitu hivi Muhimu kwako kama ni Mwanaume ili kuwa na Afya bora ya Uzazi;

- Epuka matumizi ya Pombe

- Epuka Uvutaji wa Sigara, au matumizi ya Ugoro,tumbaku n.k

- Epuka matumizi ya dawa zozote za kulevyia

- Hakikisha Unadhibiti Uzito mkubwa wa mwili

- Fanya Mazoezi ya mwili mara kwa mara,angalau kwa dakika 30 kila siku

- Epuka tabia ya kufanya Punyeto

- Epuka matumizi ya vyakula vya mafuta mengi sana au chumvi nyingi

- Endapo una magonjwa kama haya hakikisha unapata Tiba mapema;

  • Magonjwa ya Moyo
  • Ugonjwa wa kisukari
  • Ugonjwa wa Presha
  • Magonjwa ya Zinaa kama kaswende,kisonono,chlamydia n.k

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



Post a Comment

0 Comments