Ticker

6/recent/ticker-posts

Dalili za Upungufu wa vitamin d,soma hapa kufahamu



Dalili za Upungufu wa vitamin d,soma hapa kufahamu

Katika makala hii tunazungumzia tatizo la upungufu wa vitamin D mwilini yaani kwa kitaalam Vitamin D deficiency,

Kwa  ujumla, vitamin mbali mbali ni muhimu sana kwenye mwili wako na kila aina ya vitamin ina kazi zake mwilini, hapa nazungumzia mfano;

  • vitamin A,
  • Vitamin B6,
  • Vitamin C,
  • Vitamin D,
  • Vitamin B9,
  • Vitamin B12 n.k

Upungufu wa vitamin D mwilini unasababishwa na nini? Na dalili zake ni zipi?(soma makala hii)

CHANZO CHA UPUNGUFU WA VITAMIN D MWILINI NI PAMOJA NA;

- Kula vyakula ambavyo havina vitamin D  kwa muda mwingi

- Kukaa mbali na jua kwa muda mrefu kwani utengenezaji wa vitamin D mwilini mwako hutegemea pia jua.

- Figo zako kushindwa kubadilisha vitamin D kuwa katika hali ya kutumika zaidi hasa kwa watu wenye umri mkubwa

- Kuwa na ngozi nyeusi sana, tafiti zinaonyesha melanini huweza kupunguza ngozi kutengeza vitamin D pale inapopigwa na jua

- Tatizo la mfumo wako wa umeng'enyaji kushindwa kufyoza vizuri vitamin D mbali na chakula unachokula chenye vitamin vya kutosha.

DALILI ZA UPUNGUFU WA VITAMIN D MWILINI

Dalili za upungufu wa vitamin d ni pamoja na;

- Kupata maumivu ya mgongo mara kwa mara

- Kupata maumivu ya misuli,joint pamoja mifupa ya mwili mara kwa mara

- Kuwa na tatizo la vidonda kutokupona haraka

- Uchovu wa mwili kupita kiasi

-  kuwa na tatizo la Nywele kukatika sana na kunyonyoka zenyewe

- Watoto kuwa na shida ya matege

- Kushambuliwa na magonjwa mara kwa mara kutokana na kinga yako ya mwili kutokufanya kazi vizuri

N.k

TIBA YA UPUNGUFU WA VITAMIN D MWILINI

- Matibabu ya upungufu wa vitamin D mwilini huhusisha matumizi ya vyakula vyenye kiwango cha kutosha cha vitamin D, Dawa zakusaidia umeng'enyaji pamoja na ufyozwaji wa vitamin D mwilini, pamoja na matumizi ya Virutubisho mbali mbali yaani supplements

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.



Post a Comment

0 Comments