Ticker

6/recent/ticker-posts

Dida shaibu afariki dunia



Dida shaibu afariki dunia 

Mtangazaji Dida Shaibu Afariki Dunia

Mtangazaji maarufu nchini, Khadija Shaibu almaarufu Didah amefariki dunia jioni ya leo, Oktoba 4, 2024.

Taarifa za kifo cha Didah zimethibitishwa na mtangazaji mwenzake ambaye pia ni mtu wake wa karibu, Maulid Kitenge kupitia akaunti zake za mitandao ya kijamii.

Mtangazaji huyo wa Wasafi FM kupitia kipindi cha 'Mashamsham', Khadija Shaibu maarufu kama Dida amefariki Dunia usiku huu wa leo Ijumaa, Oktoba 4, 2024 baada ya kuugua na kulazwa hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Taarifa za msiba huo zimethibitishwa na mtangazaji mwenzake, Maulid Baraka Kitenge kupitia mitandao yake ya kijamii.

Kitenge ameandika; “Dida shaibu wa Wasafi FM amefariki dunia."

Didah amefikwa na umauti akiwa na umri wa miaka 42, ambapo kifo chake kimetokea siku kumi na sita (16) toka Wafuasi wake washuhudie ukimya wake katika mitandao ya kijamii ambapo chapisho lake la mwisho mtandaoni lilikuwa Septemba 19, 2024 ambapo aliweka picha yake akiwa kwenye gari ikisindikizwa na wimbo wa Martha Mwaipaja “Amenitengeneza".

Kabla ya kutua Wasafi, Dida alikuwa akifanya kazi ya utangazaji katika kituo cha Times FM kupitia kipindi cha Mirindimo.



Post a Comment

0 Comments