Ticker

6/recent/ticker-posts

Nchi ya Rwanda kuanza majaribio ya chanjo na Tiba dhidi ya Ugonjwa wa Marburg



Nchi ya Rwanda kuanza majaribio ya chanjo na Tiba dhidi ya Ugonjwa wa Marburg

Nchi ya Rwanda iko tayari kuanza majaribio ya chanjo na matibabu ya ugonjwa wa Marburg, Yvan Butera, waziri msaidizi wa afya alisema siku ya Alhamisi, huku taifa hilo la Afrika Mashariki likipambana na mlipuko wake wa kwanza wa homa hay ya virusi ambayo imewaua watu11.

“Hii ni sehemu ya juhudi zetu za kusaidia watu kupona haraka kwa kutumia chanjo na dawa zilizotengenezwa mahsusi kupambana na mlipuko huu, kwa sasa katika awamu ya mwisho ya utafiti,” waziri, Sabin Nsanzimana, aliiambia Reuters.

“Tunashirikiana na makampuni ya dawa yaliyotengeneza dawa hizi, pamoja na Shirika la Afya Ulimwenguni ili kuharakisha mchakato huo kupitia ushirikiano wa kimataifa.”

Alisema serikali inazungumza na makampuni yaliyoko Marekani na Ulaya.

Wizara hiyo ilikuwa ikifuatilia watu 410 ambao walikuwa wamewasiliana na wale walioambukizwa, aliongeza, huku i wengine watano waliopimwa wakibainika kuwa hawana, lakini walisubiri matokeo ya vipimo zaidi

Ugonjwa huo ulithibitishwa kwa mara ya kwanza mwishoni mwa Septemba, na watu 36 wameripotiwa kupata maradhi hayo hadi sasa, data ya wizara ya afya inaonyesha.



Post a Comment

0 Comments