Ticker

6/recent/ticker-posts

Wanaume wenye Vipara wakimbilia Muhimbili



Wanaume wenye Vipara wakimbilia Muhimbili

Daktari Bingwa wa Upasuaji Rekebishi na Upasuaji Urembo, Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Dk. Edwin Mrema, amesema kuwa Wataalamu wanafanya upasuaji kwa wagonjwa 12 hadi 15 kwa wiki , huku idadi kubwa ya wanaohitaji huduma ya Upasuaji rekebishi ikiwa ni wanaume wenye kipara.

Huduma zinazofanywa mara kwa mara ni pamoja na upasuaji rekebishi kwa majeruhi wa ajali za viwandani, barabarani, matukio ya moto; kukiwa na wastani wa wagonjwa sita hadi wanane kwa siku.

Dk. Mrema pia amesema mpaka sasa nchi ina wataalamu 10 ,waliobobea katika upasuaji rekebishi na upasuaji wa urembo.



Post a Comment

0 Comments