Je,Ndizi inaweza kusababisha tatizo la Choo kigumu au inaweza kuondoa tatizo la Choo kigumu?

Je,Ndizi inaweza kusababisha tatizo la Choo kigumu au inaweza kuondoa tatizo la Choo kigumu?

#1

Je,Ndizi inaweza kusababisha tatizo la Choo kigumu au inaweza kuondoa tatizo la Choo kigumu?



Watu wengi hawajui Ndizi huweza kuchangia kupata tatizo la choo kigumu au huweza kusaidia kuondoa tatizo hili la kupata choo kigumu kulingana na kiwango chake cha kukomaa.

Hapa tutaangalia vitu hivi viwili; 

(1) Kuna ndizi mbichi(Unripe bananas)

(2) Na Kuna ndizi mbivu(Ripe bananas)

Fahamu kwamba; Ndizi mbichi zina viwango vya juu vya tannins na aina ya wanga ambao tunaita resistant starch, Vitu hivi huweza kusababisha au kuzidisha tatizo la kupata choo kigumu ambalo ulikuwa nalo hapo awali.

Ndizi mbichi (ndizi ambazo hazijaiva) zina kiwango kikubwa cha wanga, hasa aina ya wanga sugu (resistant starch), ambayo ni ngumu kwa mwili kuitengeneza haraka. Hii inaweza kusababisha kuchelewesha usagaji wa chakula kwenye mfumo wa mmeng'enyo, na hivyo kufanya choo kuwa kigumu. Pia, ndizi mbichi zina kiwango kikubwa cha tanini, ambacho kinaweza kupunguza maji kwenye utumbo mkubwa, hivyo kuchangia ugumu wa choo.

Wakati Ndizi mbivu zinaweza kusaidia kuzuia au kupunguza tatizo la kupata choo kigumu kwa sababu ya kiwango kizuri cha nyuzinyuzi(fibers), mradi tu mtu huyo atumie maji ya kutosha.

Ndizi zilizoiva zina nyuzinyuzi nyingi, ambazo zinaweza kusaidia kuzuia au kupunguza tatizo la kufunga choo au kupata choo kigumu (constipation), mradi mtu anakunywa maji ya kutosha. Nyuzinyuzi husaidia kulainisha choo na kurahisisha kupita kwake kwenye mfumo wa mmeng'enyo.

Kwa Mantiki hii,Kama unashida ya kupataa choo kigumu au kukosa kabsa choo,Ndizi mbivu ni nzuri zaidi kwako!.

TOA MAONI YAKO HAPA(REPLY BELOW👇)


image quote pre code