Jukwaa la Midahalo(Discussions Corner)
Nimefanyiwa upasuaji mara 100 na siachi’ Nini Ushauri wako hapa
Nimefanyiwa upasuaji mara 100 na siachi’ Nini Ushauri wako hapa
Abby Wu alikuwa na umri wa miaka 14 tu alipofanyiwa upasuaji wa urembo bandia kwa mara ya kwanza.
Baada ya kupata matibabu ya homoni, uzito wa mwili wa Abby uliongezeka kutoka kilo 42 hadi kilo 62 ndani ya miezi miwili.
Mwalimu wake wa michezo ya kuigiza aligundua mabadiliko hayo ya mwili.
Mwalimu wangu aliniambia, ”ulikuwa nyota lakini sasa umekuwa mnene kupita kiasi. Chagua moja uondoke kwa tasnia hii au upunguze kilo,” anakumbuka alichoambiwa kipindi hicho akisubiri kufanya mtihani wake wa tamthilia.
Mama yake Abby aliingilia kati na kuamua kumpeleka kufanyiwa upasuaji wa kuondoa mafuta tumboni na miguuni.
Abby anavuta kumbukumbu jinsi mamake alivyompa motisha akisubiri kufanyiwa operesheni hiyo.
”Kuwa mkakamavu na uingie ufanyiwe. Ukitoka hapo utakuwa mrembo zaidi.”
Upasuaji huo ulimuacha na makovu. Abby alipatiwa dawa za kupunguza uchungu lakini alikuwa macho akifanyiwa operesheni hiyo.
”Ningeona kiasi cha mafuta kilichotolewa mwilini mwangu na damu iliyokuwa ikinivuja,” anasema.
“Upasuaji ulifanya kazi. Nilijiamini na kuwa na furaha zaidi, siku baada ya siku. Nadhani mama yangu alifanya chaguo sahihi.”
Sasa Abby ana umri wa miaka 35 na amefanyiwa upasuaji wa urembo mara mia moja ikimgharimu dola nusu milioni.
Anamiliki kliniki ya ulimbwende katikati mwa mji wa Beijing na amekuwa mtu tajika katika tasnia ya upasuaji wa plastiki nchini China.
Lakini upasuaji huo pia unaathari zake kwa mwili.
Akiwa amekaa mbele ya kioo anajipodoa ili kuficha makovu ya sindano za kupunguza unene usoni, utaratibu anaoufanya kila mwezi ili kuhakikisha uchanga usoni mwake nakuhakikisha hana ngozi zilizolegea baada ya upasuaji wa kupunguza taya uliondoa mifupa mingi.
Lakini anasisitiza kuwa hajutii upasuaji wa urembo aliyofanya kufikia sasa akiamini kuwa mamake hakukosea kumuanzisha katika ulimbwende huu.
500
Atumia siku 1,500 kukuza nywele ili kumsaidia mchumba wake wenye alopecia
Atumia siku 1,500 kukuza nywele ili kumsaidia mchumba wake wenye alopecia
Mwanamume huyu alitumia karibu siku 1,500 kukuza nywele zake akiwa na lengo moja mahususi akilini: kumpa mchumba wake wigi la asili linalobeba sehemu yake. Uamumizi huo ni kumsaidia mchumba wake mwenye tatizo la nywele kutokuota kichwani au alopecia.
Hapo Vipi? Wanaume😂😂
#love #relationshipgoals #alopecia
Jukwaa la Midahalo(Discussions Corner)
Breaking: Chukueni tahadhari dhidi ya uwepo wa COVID 19
Breaking: Chukueni tahadhari dhidi ya uwepo wa COVID 19
Wizara ya Afya imesema imeendelea kufanya ufuatiliaji wa karibu na kutoa taarifa za kila siku kuhusu magonjwa ya mlipuko pamoja na tetesi za uwepo wa magonjwa hayo nchini ambapo imesema tangu February hadi April 2025, ufuatiliaji wa virusi vya Covid 19 umeonesha ongezeko la maambukizi kutoka 1.4% (Wagonjwa wawili kati ya Watu 139 waliopimwa) mwezi February hadi 16.3% (Wagonjwa 31 kati ya 190 waliopimwa) mwezi March, na kisha 16.8% (Wagonjwa 31 kati ya Watu 185 waliopimwa) mwezi Aprili 2025.
Taarifa iliyotolewa leo May 20,2025 na Mganga Mkuu wa Serikali, Dkt. Grace Magembe imesema “Ugonjwa wa UVIKO-19, ambao ulitangazwa kwa mara ya kwanza nchini March 2020, umeendelea kuwepo kwa kiwango cha chini kama yalivyo magonjwa mengine ya mfumo wa njia ya hewa, hali ya kuongezeka na kupungua kwa ugonjwa huu imekuwepo kila mwaka tangu kutangazwa kwa ugonjwa huu mwaka 2020, kwa kipindi hiki ongezeko hili linaonekana zaidi katika Mkoa wa Dar es salaam, Wizara ya Afya inaendelea kufuatilia kwa karibu mwenendo wa magonjwa ya mfumo wa njia ya hewa nchini na kutoa taarifa”
“Katika kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi Aprili 2025, tumeshuhudia ongezeko la tetesi zinazohusiana na magonjwa ya mfumo wa njia ya hewa katika jamii hapa nchini, hasa katika mkoa wa Dar es salaam, kwa kutumia mifumo ya ufuatiliaji wa magonjwa ya mfumo wa njia ya hewa, ambayo imekuwepo tangu mwaka 2008, tumekuwa tukifuatilia mwenendo wa magonjwa haya ili kubaini aina za vimelea vinavyosababisha maambukizi, ongezeko la visa, pamoja na uwezekano wa kujitokeza kwa kirusi kipya chenye uwezo wa kusambaa kwa haraka”
“Vipimo vya maabara vimebaini kuongezeka na kupungua kwa virusi vya influenza hali ambayo imekuwa ikionekana pia katika miaka iliyopita na ndiyo maana hujulikana kama ‘Seasonal influenza”, vipimo vimeonesha kuwa hakuna kirusi kipya kinachoweza kusambaa kwa haraka na kusababisha mlipuko wa aina ya Pandemiki” Cc:MillardAyoUPDATES
Jukwaa la Midahalo(Discussions Corner)
Hatimaye majibu ya vinasaba (DNA) yaliyokuwa yanasubiriwa yametolewa
Hatimaye majibu ya vinasaba (DNA) yaliyokuwa yanasubiriwa yametolewa
Hatimaye majibu ya vinasaba (DNA) ya watoto watatu waliozaliwa Machi 24, 2025 katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Arusha (Mount Meru) yametolewa, huku Neema Kilugala, mkazi wa mtaa wa Ndaravoi, Kata ya Daraja Mbili jijini Arusha, akiangua kilio baada ya kutoridhishwa na matokeo hayo.
Neema ambaye alijifungua kwa upasuaji katika hospitali hiyo, alidai kuwa alibadilishiwa mtoto na hakuwahi kuridhika na mtoto aliyekabidhiwa, akisema mtoto wake alizaliwa akiwa mzima wa afya na mwenye uzito wa zaidi ya kilo tatu.
Akizungumza kwa uchungu nje ya Kituo Kikuu cha Polisi mkoani Arusha Aprili 3, 2025, Neema alisema anaamini kuwa mtoto wake yupo hai na kuna mwanamke mwingine aliyepewa mtoto wake kwa bahati mbaya au makusudi.
Mama mzazi wa Neema naye alilia kwa uchungu, akiitaka serikali irejee upya vipimo vya DNA kwa watoto wote watatu, kwa kuwa mtoto ambaye inadaiwa ni wa binti yake (Neema) na tayari ameshafariki, si wake kwa mujibu wa maumbile na hisia zao za kizazi.
Kutokana na utata huo, serikali iliamuru kufanyika kwa vipimo vya DNA kwa wanawake wote waliowajifungua watoto siku hiyo pamoja na watoto wao, ili kupata ukweli wa jambo hilo.
Kwa mujibu wa Afisa Sheria kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Bw. George Daniel, ambaye yupo jijini Arusha kupitia kampeni ya “Samia Legal Aid”, alisema walipokea wito kutoka Polisi kwa ajili ya kushiriki katika kusikiliza majibu ya vinasaba hivyo.
“Katika matokeo haya, ambapo wazazi wote watatu walikuwepo, vipimo vimeonyesha kwa asilimia zaidi ya 99 kuwa mtoto anayelalamikiwa na Neema kuwa si wake, ndiye mtoto wake halisi kwa mujibu wa vinasaba,” alisema Bw. Daniel.
Aliongeza kuwa, iwapo Neema bado anahitaji msaada wa kisheria, ofisi yao iko tayari kumsaidia kupitia kampeni ya Samia Legal Aid ambayo inalenga kuwasaidia wananchi wanyonge kupata haki zao.
Diwani wa Kata ya Daraja Mbili aliyefika kituoni hapo pamoja na familia ya Neema alisema kuwa wataitisha kikao cha pamoja kujadiliana hatua za kuchukua kufuatia matokeo hayo.
Kwa upande wake, Makamu wa Rais wa Chama cha Wauguzi Tanzania (TANNA) alitoa wito kwa wauguzi nchini kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi, akibainisha kuwa chama hicho kitaendelea kufuatilia kwa karibu utendaji kazi wa wauguzi kuhakikisha haki na uadilifu vinaendelea kutawala katika huduma za afya.
-
magonjwa2 years ago
Muwasho sehemu za siri kwa mwanaume chanzo chake
-
afya5 years agoCHANZO CHA TATIZO LA KUPASUKA MIGUU KWENYE KISIGINO(gaga)
-
Madhara ya mtoto kunywa maji machafu2 weeks ago
Madhara ya mtoto kunywa maji machafu au maji ya uzazi
-
Madhara ya mtoto kunywa maji machafu2 weeks ago
Madhara ya Mtoto Kunywa Maji Machafu: Dalili, Hatari na Namna ya Kumsaidia
-
Madhara ya Pombe1 week agoJE, POMBE hupunguza testosterone na Ubora wa mbegu za Kiume?
-
afya5 years agoDawa za Kukausha kidonda,kuzuia maambukizi Na SABABU za Kidonda Kutokupona Haraka
-
Afya News1 week agoDaktari amfanyia Upasuaji Mama kumtoa Mtoto ili kumfanyia upasuaji wa Uvimbe Kisha Kumrudisha tena tumboni
-
choo chenye makamasi1 week ago
Choo chenye makamasi,chanzo cha kujisaidia choo chenye makamasi au Usaha

