TANZIA: Mwigizaji Caren afariki Dunia
Mwigizaji Caren amefariki Dunia leo April 15,2025 akiwa anapatiwa matibabu nchini India kutokana na maradhi ya tumbo yaliyokuwa yakimsumbua kwa muda wa zaidi ya miaka 8 .
Taarifa hizo zimethibitishwa na Mdogo wake Safinewin Rwegasira ambaye alienda nae India licha ya kuwa yeye aliwahi kurudi kwa ajili ya kumuangalia Mama yao ambaye ni Mgonjwa pia.
Mdogo wa Careen amesema mara ya mwisho kuongea na Dads yake ilikuwa usiku wa kuamkia leo na alikuwa kwenye hali nzuri tu alimuahidi Mama yao kuwa hatamani kufariki ili arejee mzima aweze kutimiza yale aliyoahidi.
“Nimeongea nae, alikuwa yuko vizuri tu Dada yangu akawa anaongea na Mama anamwambia Mama yangu naomba Mungu nisife kabla yako, sijatimiza ahadi zangu zote nilizokuahidi, alikuwa anatarajiwa kurudi tarehe 22, alikuwa amemaliza operation zote”