Wananchi wa Tanzania wanapaswa kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa saratani ili waweze kuwa salama, kutokana na idadi ya vifo vinavyotokana na ugonjwawa saratani kuwa kubwa kidunia.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya Dkt. JenisterMhagama, katika maadhimisho ya Samia SaluhuOustreach ambao wameweka kambi kwaajili yauchunguzi wa Saratani, Iliyofanyika katika hospitali yaPeramiho iliyopo Halmashauri ya Peramiho wilaya yaSongea, Mkoani Ruvuma. Na kuwasisitiza kujinga naUgonjwa huo wa Saratani.
Amesema, “Athari za ugonjwa wa saratani kiduniakama nilivyosema mwanzo zimekuwa zikiongezeka, natakwimu za mwaka 2018 zinaonyesha kuwa kiduniakati ya watu sita wanaokufa, mmoja amekufakwasababu ya saratani.”
Aidha ameongeza kwa kusema kuwa athari hizo kamakusipokuwa na mpango mahususi wa kuzuia vifo hivimpaka mwaka 2030 vinaweza kuwa vimeongezeka.
“Tushirikiane wote kuhakikisha kwamba tunapambanakuzuia hivyo vifo lakini ikiwezekana tupambanekuzuia ugonjwa wa saratani katika nchi yetu yatanzania. Ili tuweze kuwa salama tuweke msisitizokwenye kinga, tuzingatie ulaji unaofaa na hasa kwakuongeza kula mbogamboga, matunda ya kutoshambogamboga nyingi, tupunguze kula vyakula vyenyemafuta, tupunguze chumvi nyingi kwenye chakula, tupunguze kula sukari, tuitikie wito wa mh. raisi kwakufanya mazoezi.”
Aidha Mhagama, kupitia maadhimisho hayo yasaratani, aliwaasa wananchi kujikinga na magonjwamengine ya mlipuko ambayo mengi yanatokana namuingiliano kati ya wanyama pamoja na Binadamukutokana na kuwa na ongezeko kubwa la idadi ya watupamoja na uharibifu wa mazingira. Amesema,
“Dunia hii inakwenda kwa haraka kwa speed, mabadiliko ni makubwa sana, zamani ilikuwa ukisikiamtu anaugua labda ni malaria, ama surua, magonjwa kama ya polio ambayo tumeshakwisha kuitokomezakatika nchi kwetu,” amesema na kuongeza
“Lakini ongezeko la idadi ya watu duniani, ukijumlishana uharibifu wa mazingira, kumeanza kuwa namuingiliano kati ya binadamu na wanyama wa polini, siku hizi wala huoni ajabu nyani wanakuja kukaa mpaka kwenye nyumba za watu, wamehama porini nikwa sababu ya uharibifu wa mazingira, binadamu wamewaingilia wanyama na wanyama wamewaingilia binadamu.
“Matokeo yake ongezeko la magonjwa mapya ya mlipuko yanayoambukizwa limekuwa nikubwa, huu ni upande mmoja wa dunia tunayoishisasa, na ndiyo maana sasa hivi tunawaambia tuna homaya epoxi homa ya nyani, huko nyuma ungeshangaakusikia kuna homa ya nyani, lakini siku hizi kunahoma ya nyani imeingia kwa bindamu. na niendeleekuwaomba wananchi wa mkoa wa ruvuma kuendeleakuchukua tahadhari.” amesema
Reply
image quote pre code