Connect with us

WHO

WHO yapigia chapuo matumizi ya Usafiri wa Baiskeli duniani

Doctor Ombeni

Published

on

100 Views
0 Comments

WHO yapigia chapuo matumizi ya Usafiri wa Baiskeli duniani


Shirika la Afya Duniani WHO, limetoa wito mpya kwa nchi zote duniani kutumia baiskeli kama njia muhimu ya kukuza afya, kulinda mazingira na kuendeleza maendeleo endelevu, wakati dunia ikiadhimisha Siku ya Baiskeli Duniani leo.

Siku ya Baiskeli Duniani ilianzishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwaka 2018 ili kutambua baiskeli kama chombo cha usafiri “rahisi, nafuu, cha kuaminika na kisicho haribu mazingira.”

Azimio hilo, lililoletwa na Serikali ya Turkmenistan, linatambua mchango wa baiskeli katika kuendeleza malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) kupitia usafiri safi na jumuishi.

WHO imesisitiza kuwa baiskeli ina nafasi muhimu zaidi hasa baada ya janga la coronavirus”>COVID-19, ambapo miji mingi duniani inatafuta mifumo ya usafiri iliyo na uimara zaidi na isiyochafua mazingira. “Kutumia baiskeli kunapunguza uchafuzi wa hewa na msongamano wa magari, huku kukisaidia afya ya moyo, kupunguza hatari ya magonjwa kama saratani na kisukari, na kuboresha afya ya akili,” imesema WHO.

Azimio la pili latoa msukumo mpya kwa usafiri wa baiskeli

Mwaka 2022, Umoja wa Mataifa ulipitisha azimio la pili linalohamasisha mataifa kuingiza baiskeli katika mifumo yao ya usafiri wa umma. Azimio hilo linahimiza uboreshaji wa miundombinu ya barabara ili iwe salama kwa watumiaji wote, na kuendeleza utamaduni wa kupanda baiskeli katika maeneo ya mijini na vijijini.

WHO pia imetoa nyenzo mpya mwaka huu kusaidia nchi na miji kuboresha usalama wa barabarani na kuongeza matumizi ya baiskeli. Nyenzo hizo ni pamoja na miongozo ya sera, vifaa vya afya ya umma na nyaraka za elimu.

Baiskeli kama chombo cha mabadiliko ya kijamii

“Baiskeli siyo tu njia ya usafiri,” amesema msemaji wa WHO akiongeza kuwa “Ni chombo chenye uwezo wa kupunguza ukosefu wa usawa, kukuza elimu, kujumuisha jamii, na kujenga utamaduni wa amani.”

Siku ya Baiskeli Duniani inaendelea kuvutia usaidizi kutoka kwa wanaharakati, viongozi wa miji, na wataalamu wa afya, wanaoamini kuwa baiskeli ni gari la mabadiliko ya kijamii na mazingira duniani kote.

100 Views
0 Comments

Medical Disclaimer

Medical Disclaimer: Taarifa kwenye makala hii ni kwa ajili ya Updates au elimu ya jumla tu na haichukui nafasi ya uchunguzi,Tiba au ushauri wa kitaalamu wa daktari kwa mtu mmoja mmoja. Kama una dharura au tatizo lolote la kiafya, tafadhali Wasiliana na Daktari moja kwa moja hapa.

Je, unahitaji ushauri binafsi au matibabu ya tatizo lolote?

💬 Wasiliana na Daktari Hapa

🏆Certified| Doctor from Afyaclass. Maudhui haya ni kwa ajili ya elimu ya jumla ya afya. Unapohitaji ushauri wa kina, uchunguzi, au matibabu binafsi, wasiliana na daktari kupitia namba:+255758286584.Pia tufwatilie kupitia: @Facebook | @Instagram | @YouTube.

LATEST POSTS

magonjwa1 year ago

Ugonjwa wa genital warts,Chanzo,Dalili na Tiba

Ugonjwa wa genital warts,Chanzo,Dalili na Tiba Genital warts ni ugonjwa gani,Soma Zaidi hapa kufahamu Genital warts ni moja ya aina...

magonjwa2 years ago

Vipele Sehemu Ya Siri,Vipele Ukeni, Vipele Kwenye Uume

VIPELE SEHEMU YA SIRI,VIPELE UKENI, VIPELE KWENYE UUME Vipele kwenye Uume: Vipele Kwenye Uume: Chanzo, Dalili na Matibabu Tatizo la...

magonjwa ya wanawake5 years ago

PID NI NINI? Na Dalili zake ni Zipi?(magonjwa ya Wanawake)

 PID • • • • • PID NI NINI? Na Dalili zake ni Zipi?(magonjwa ya Wanawake) PID NI NINI?  PID...

afyatips1 day ago

Dalili za kidonda cha operation kupona

DALILI ZA KIDONDA CHA OPERATION KUPONA Baada ya kufanyiwa operation, mwili huanza mchakato wa kuponya kidonda mara moja. Mchakato huu...

Utafiti1 day ago

Desogestrel yahusishwa na Kuongezeka kwa Hatari ya uvimbe wa ubongo

Mamlaka ya Dawa na Bidhaa za Afya ya Ufaransa (ANSM) imewaonya wanawake wanaotumia baadhi ya njia za uzazi wa mpango...

magonjwa5 years ago

UGONJWA WA BRUCELLA(chanzo,dalili na tiba)

UGONJWA WA BRUCELLA(chanzo,dalili na tiba) Huu ni ugonjwa ambao kwa kitaalam hujulikana kama brucellosis na chanzo chake ni bacteria wanaojulikana...

magonjwa ya watoto2 years ago

Ugonjwa wa Surua kwa Watoto: Sababu, Dalili, Matibabu na Kinga

Ugonjwa wa Surua kwa Watoto: Sababu, Dalili, Matibabu na Kinga Ugonjwa wa Surua ni ugonjwa wa kuambukiza sana kwa watoto...

Afya News2 days ago

Vifo vya Watoto Wachanga Katika Mlipuko wa Surua Pennsylvania na Mjadala wa Afya ya Umma

Mlipuko wa ugonjwa wa surua (measles) unaoendelea katika jimbo la Pennsylvania, Marekani, umeendelea kuzua wasiwasi mkubwa baada ya watoto wawili...

Afya News2 days ago

Wauguzi Kenya Wasitisha Mgomo Baada ya Makubaliano na Serikali

Wauguzi nchini Kenya wamesitisha mgomo wao wa siku 43 baada ya kufikia makubaliano na serikali kupitia chama chao cha wafanyakazi....

WHO3 days ago

Uvutaji Sigara Unaongeza Uwezekano wa Ugumba

Uvutaji Sigara Unaongeza Uwezekano wa Ugumba Shirika la Afya Duniani (WHO) limeonya kuwa matumizi ya tumbaku yana athari kubwa kwa...

101
0