Afya News
Mimba za Utotoni zapungua kwa Mkoa wa Iringa,Ripoti Mpya
Shirika la SOS Children’s Village limefanikiwa kupunguza kwa kiasi kikubwa matukio ya mimba za utotoni kwa wasichana mkoani Iringa, kutoka asilimia 18 mwaka 2020 hadi kufikia asilimia 15 mwaka 2024, kupitia utekelezaji wa mradi wa Mabinti Bora unaolenga kuimarisha malezi na elimu kwa watoto.
Mradi huo umefadhiliwa na Serikali ya Finland kupitia Wizara ya Mambo ya Nje ya nchi hiyo, na kuhusisha wadau mbalimbali wakiwemo wataalamu wa serikali kutoka idara za elimu na maendeleo ya jamii.
Akizungumza katika kikao kazi cha kupitia sera za vijana na changamoto zake, Meneja wa Mradi huo, Victor Mwaipangu, alisema kuwa kabla ya kuanza kwa mradi huo, takwimu zilionesha asilimia 18 ya wasichana wenye umri wa miaka 15 hadi 18 walikuwa wakipata mimba za utotoni, hali iliyowapelekea wengi kushindwa kuendelea na masomo.
“Takwimu za kitaifa zinaonesha asilimia 22 ya wasichana hupata mimba za utotoni. Kwa Iringa tulianza na asilimia 18 lakini kwa sasa Manispaa ya Iringa imepungua hadi chini ya asilimia 10, huku wilaya za Mafinga na Mufindi zikiwa kwenye asilimia 10 na 12,” alifafanua Mwaipangu.
Amesema kupitia ushirikiano na walimu, maafisa wa maendeleo ya jamii na viongozi wa shule, waliweza kutoa elimu ya malezi, haki na wajibu wa watoto kwa wanafunzi, wazazi na walimu katika shule mbalimbali mkoani humo.
“Tulianza na matukio 36 ya mimba kwa mwaka, lakini sasa matukio hayo yamepungua hadi kufikia kati ya sita hadi nane kwa mwaka,” alisema.
Mbali na mradi wa Mabinti Bora, Mwaipangu alisema shirika hilo pia liliwahi kutekeleza mradi wa kuwawezesha wanawake kiuchumi na kuelimisha kuhusu haki za watoto, ambao uliwanufaisha wanawake 250 wa Mufindi waliokuwa wakilea watoto zaidi ya 1,000.
Pia walitekeleza mradi wa elimu katika shule nane wilayani Iringa uliolenga kuboresha miundombinu ya kujifunzia, ikiwemo ujenzi wa vyoo na ukarabati wa madarasa, jambo lililopelekea baadhi ya shule zilizokuwa zikishika nafasi za mwisho kitaaluma, kupanda hadi nafasi ya tatu bora kwa ngazi ya wilaya.
Kwa upande wake, Afisa Mradi kutoka SOS Children’s Village, Benson Lwakatare, alisema kikao kazi hicho kilishirikisha maafisa kutoka Wizara ya Afya, Elimu, TAMISEMI, na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, pamoja na viongozi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa.
Lwakatare alieleza kuwa lengo kuu la kikao hicho ni kupitia sera zilizopo zinazohusu vijana, kuangalia changamoto katika utekelezaji wake, na kutafuta njia bora za kuimarisha maisha ya vijana kupitia miradi yenye tija.
“Ni muhimu kuhakikisha sera zinaendana na uhalisia wa maisha ya vijana wetu, ili miradi tunayotekeleza iwe na matokeo chanya na ya kudumu,” alisisitiza.
Afya News
Daktari amfanyia Upasuaji Mama kumtoa Mtoto ili kumfanyia upasuaji wa Uvimbe Kisha Kumrudisha tena tumboni
Afya News
Daktari Aliyerudi Kutoka Congo Agundulika na Ebola Nchini Ufaransa
Daktari Aliyerudi Kutoka Congo Agundulika na Ebola Nchini Ufaransa
Mamlaka za afya nchini Ufaransa zimethibitisha kisa cha Ebola kwa daktari aliyerejea hivi karibuni kutoka katika misheni ya kibinadamu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Kwa mujibu wa Wizara ya Afya ya Ufaransa, mgonjwa huyo amewekwa kwenye uangalizi maalum wa kutengwa (isolation) huku maafisa wa afya wakianza kuwatafuta watu wote ambao huenda walikutana naye baada ya kuwasili nchini humo.
Mamlaka zimeeleza kuwa hatari ya maambukizi kwa wananchi wa Ufaransa na Ulaya kwa ujumla bado ni ndogo kutokana na hatua kali za ufuatiliaji na udhibiti zinazochukuliwa.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), , amesema hakuna sababu ya taharuki. Akizungumza na waandishi wa habari, Tedros alieleza kuwa katika kipindi cha zaidi ya miaka 50 iliyopita, chini ya visa 30 vya Ebola vimewahi kuripotiwa nje ya bara la Afrika.
Wakati huo huo, mlipuko wa Ebola unaoendelea nchini umehusishwa na aina adimu ya virusi vya Bundibugyo. Shirika la Afya Duniani limesema mlipuko huo umeambukiza zaidi ya watu 1,000 na kusababisha vifo vya watu 267.
Wataalamu wa afya wanaamini kuwa virusi hivyo huenda vilianza kusambaa kwa miezi kadhaa kabla ya mamlaka kutangaza rasmi mlipuko huo mnamo Mei 15, 2026. Visa vya awali viligunduliwa katika maeneo ya mijini, na baadaye maambukizi kuripotiwa katika kambi kadhaa zenye idadi kubwa ya wakimbizi na watu waliokimbia makazi yao.
Ebola ni Ugonjwa Gani?
Ebola ni ugonjwa hatari unaosababishwa na virusi vya Ebola. Ugonjwa huo huambukizwa kupitia kugusana moja kwa moja na damu, majimaji ya mwili au tishu za mtu aliyeambukizwa au aliyefariki kutokana na ugonjwa huo.
Dalili zake ni pamoja na:
- Homa kali
- Maumivu ya kichwa
- Uchovu mkubwa
- Maumivu ya misuli
- Kutapika
- Kuharisha
- Kutokwa damu katika baadhi ya wagonjwa
Soma Zaidi:Ugonjwa wa Ebola hapa
WHO inaeleza kuwa ugonjwa huu unaweza kuwa hatari sana ikiwa hautagunduliwa na kutibiwa mapema.
Takwimu Muhimu
- Zaidi ya watu 1,000 wameambukizwa katika mlipuko wa sasa nchini Congo.
- Watu 267 wamefariki dunia.
- Chini ya visa 30 vya Ebola vimeripotiwa nje ya Afrika katika kipindi cha zaidi ya miaka 50.
- Hatari kwa Ulaya imeelezwa kuwa ndogo na WHO pamoja na mamlaka za afya za Ufaransa.
#Ebola #Afya #WHO #Congo #Ufaransa #Virusi #HabariZaAfya #Tanzania
Reference;
Reuters: https://www.reuters.com/
WHO: https://www.who.int/news-room/fact-sheets/detail/ebola-virus-disease
CDC: https://www.cdc.gov/ebola/
Wikipedia (Ebola virus disease): https://en.wikipedia.org/wiki/Ebola_virus_disease
Afya News
Apandishwa Cheo kwa Kumnyonyesha Mtoto mwenye tatizo la Utapiamlo
Afisa wa polisi wa Argentina Celeste Ayala alipata kutambuliwa kimataifa baada ya kitendo cha huruma kilichowagusa mamilioni ya watu kote ulimwenguni.
Akiwa kazini katika hospitali ya watoto, Ayala alikutana na mtoto mwenye utapiamlo ambaye alikuwa ametenganishwa na mama yake na alikuwa akilia kwa njaa. Baada ya kupata ruhusa kutoka kwa wafanyakazi wa matibabu, alimnyonyesha mtoto huyo, licha ya kutokuwa na uhusiano wowote wa kibinafsi na mtoto huyo.
Picha yake ilisambaa haraka, huku wengi wakimsifu huruma yake, wema, na nia ya kumsaidia mtoto aliye katika mazingira magumu anayehitaji Msaada. Picha hiyo imekuwa ishara yenye nguvu ya ubinadamu na huruma zaidi ya majukumu ya sare yake.
Kufuatia kutrend kwa tukio hilo, Ayala alipandishwa cheo hadi Sajenti, huku maafisa wakitaja kujitolea kwake na huduma yake kuwa vya mfano wa kuigwa.
Hadithi yake inatumika kama ukumbusho kwamba wakati mwingine vitendo vyenye maana zaidi vya utumishi wa umma havipimwi kwa cheo au mamlaka, bali kwa vitendo rahisi vya huruma ya kibinadamu.
-
magonjwa2 years ago
Muwasho sehemu za siri kwa mwanaume chanzo chake
-
afya5 years agoCHANZO CHA TATIZO LA KUPASUKA MIGUU KWENYE KISIGINO(gaga)
-
Madhara ya mtoto kunywa maji machafu2 weeks ago
Madhara ya mtoto kunywa maji machafu au maji ya uzazi
-
Madhara ya mtoto kunywa maji machafu2 weeks ago
Madhara ya Mtoto Kunywa Maji Machafu: Dalili, Hatari na Namna ya Kumsaidia
-
Madhara ya Pombe1 week agoJE, POMBE hupunguza testosterone na Ubora wa mbegu za Kiume?
-
afya5 years agoDawa za Kukausha kidonda,kuzuia maambukizi Na SABABU za Kidonda Kutokupona Haraka
-
Afya News1 week agoDaktari amfanyia Upasuaji Mama kumtoa Mtoto ili kumfanyia upasuaji wa Uvimbe Kisha Kumrudisha tena tumboni
-
choo chenye makamasi1 week ago
Choo chenye makamasi,chanzo cha kujisaidia choo chenye makamasi au Usaha


