Connect with us

Story

Furaha Chilambo wa Mtwara Mikindani, ajifungua watoto watano kwa wakati mmoja

Avatar

Published

on

115 Views
0 Comments

Furaha Chilambo wa Mtwara Mikindani, ajifungua watoto watano kwa wakati mmoja

Furaha Chilambo, mwenye umri wa miaka 32 na mkazi wa Kata ya Mtawanya, Mtaa wa Mangamba, Manispaa ya Mtwara Mikindani, amejifungua watoto watano kwa wakati mmoja katika Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kusini – Mtwara.

Furaha na mume wake, Said Hamisi, wamepokea kwa furaha ujio wa watoto hao, ambao ni mmoja wa kike na wanne wa kiume, na kufanya jumla ya watoto wao kufikia saba.

Kwa mujibu wa Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Wanawake na Uzazi katika Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kusini, Dkt. Harry Mwambe, Furaha alijifungua Agosti 7, 2026, kwa ushirikiano wa jopo la madaktari, wakunga na wahudumu wengine wa afya.

Naye Mkunga Bobezi wa Hospitali ya Rufaa Kanda ya Kusini, Cresensia Mlelwa, amesema ujauzito wa watoto watano ulikuwa na changamoto, lakini kutokana na juhudi, weledi na ushirikiano wa madaktari, wakunga na wauguzi, mama huyo amefanikiwa kujifungua salama.

Amesema kwa sasa hali ya afya ya mama na watoto hao inaendelea kuimarika.

Pamoja na furaha ya kupata watoto hao watano, Furaha na mume wake wameomba Serikali, taasisi mbalimbali, wadau wa maendeleo na wananchi wenye moyo wa kusaidia kuwafikia na kuwasaidia katika malezi ya watoto hao.

Wamesema mahitaji ya kulea watoto saba ni makubwa ikilinganishwa na kipato chao, hivyo wanaomba msaada wa mahitaji muhimu kwa watoto pamoja na mtaji utakaowawezesha wazazi hao kufanya shughuli za kiuchumi na kugharamia mahitaji ya familia.

115 Views
0 Comments

Medical Disclaimer

Medical Disclaimer: Taarifa kwenye makala hii ni kwa ajili ya Updates au elimu ya jumla tu na haichukui nafasi ya uchunguzi,Tiba au ushauri wa kitaalamu wa daktari kwa mtu mmoja mmoja. Kama una dharura au tatizo lolote la kiafya, tafadhali Wasiliana na Daktari moja kwa moja hapa.

Je, unahitaji ushauri binafsi au matibabu ya tatizo lolote?

💬 Wasiliana na Daktari Hapa

Karibu Afyaclass Jukwaa linaloongoza kwa utoaji wa elimu sahihi ya Afya. Hapa utapata Elimu na Updates mbali mbali za Afya Duniani. Pia Pata dondoo za afya kila siku kwa kufuatilia kupitia Mitandao hii hapa: @Facebook | @Instagram | @YouTube.

LATEST POSTS

magonjwa1 year ago

Ugonjwa wa genital warts,Chanzo,Dalili na Tiba

Ugonjwa wa genital warts,Chanzo,Dalili na Tiba Genital warts ni ugonjwa gani,Soma Zaidi hapa kufahamu Genital warts ni moja ya aina...

magonjwa2 years ago

Vipele Sehemu Ya Siri,Vipele Ukeni, Vipele Kwenye Uume

VIPELE SEHEMU YA SIRI,VIPELE UKENI, VIPELE KWENYE UUME Vipele kwenye Uume: Vipele Kwenye Uume: Chanzo, Dalili na Matibabu Tatizo la...

magonjwa ya wanawake5 years ago

PID NI NINI? Na Dalili zake ni Zipi?(magonjwa ya Wanawake)

 PID • • • • • PID NI NINI? Na Dalili zake ni Zipi?(magonjwa ya Wanawake) PID NI NINI?  PID...

afyatips1 day ago

Dalili za kidonda cha operation kupona

DALILI ZA KIDONDA CHA OPERATION KUPONA Baada ya kufanyiwa operation, mwili huanza mchakato wa kuponya kidonda mara moja. Mchakato huu...

Utafiti1 day ago

Desogestrel yahusishwa na Kuongezeka kwa Hatari ya uvimbe wa ubongo

Mamlaka ya Dawa na Bidhaa za Afya ya Ufaransa (ANSM) imewaonya wanawake wanaotumia baadhi ya njia za uzazi wa mpango...

magonjwa5 years ago

UGONJWA WA BRUCELLA(chanzo,dalili na tiba)

UGONJWA WA BRUCELLA(chanzo,dalili na tiba) Huu ni ugonjwa ambao kwa kitaalam hujulikana kama brucellosis na chanzo chake ni bacteria wanaojulikana...

magonjwa ya watoto2 years ago

Ugonjwa wa Surua kwa Watoto: Sababu, Dalili, Matibabu na Kinga

Ugonjwa wa Surua kwa Watoto: Sababu, Dalili, Matibabu na Kinga Ugonjwa wa Surua ni ugonjwa wa kuambukiza sana kwa watoto...

Afya News2 days ago

Vifo vya Watoto Wachanga Katika Mlipuko wa Surua Pennsylvania na Mjadala wa Afya ya Umma

Mlipuko wa ugonjwa wa surua (measles) unaoendelea katika jimbo la Pennsylvania, Marekani, umeendelea kuzua wasiwasi mkubwa baada ya watoto wawili...

Afya News2 days ago

Wauguzi Kenya Wasitisha Mgomo Baada ya Makubaliano na Serikali

Wauguzi nchini Kenya wamesitisha mgomo wao wa siku 43 baada ya kufikia makubaliano na serikali kupitia chama chao cha wafanyakazi....

WHO3 days ago

Uvutaji Sigara Unaongeza Uwezekano wa Ugumba

Uvutaji Sigara Unaongeza Uwezekano wa Ugumba Shirika la Afya Duniani (WHO) limeonya kuwa matumizi ya tumbaku yana athari kubwa kwa...

116
0