Hospital
Ugonjwa wa Homa ya Ini unaoweza kukaa mwilini kwa miaka bila dalili
Ugonjwa wa Homa ya Ini unaoweza kukaa mwilini kwa miaka bila dalili
Virusi vya Homa ya Ini vinaweza kukaa mwilini kwa muda mrefu bila kuonesha dalili, huku vikiendelea kuliharibu ini na kuongeza hatari ya kupata ugonjwa wa saratani.
Onyo hilo lilitolewa na Daktari Bingwa Mbobezi wa Magonjwa ya Mfumo wa Chakula na Ini katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, nchini Tanzania Dkt. Swalehe Kitabu Pazi, katika siku ya maadhimisho ya Siku ya Homa ya Ini Duniani tarehe 28 Julai inayolenga kutoa elimu kwa umma kuhusu ugonjwa huo.
Katika mahojiano maalum na idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa Dkt. Pazi amesema homa ya ini husababishwa na virusi vya aina mbalimbali, lakini virusi vya homa ya ini B na C ni miongoni mwa vinavyoweza kusababisha madhara makubwa visipotibiwa.
“Unaweza ukahisi kwamba uko salama, lakini ugonjwa unaendelea kuchukua hatua mbalimbali katika mwili,” amesema.
Ameeleza kuwa kugundua ugonjwa mapema humwezesha mgonjwa kuanza kufuatiliwa na kupata matibabu kabla ini halijapata madhara makubwa.
Saratani ya ini inapogunduliwa katika hatua za mwanzo inaweza kutibiwa, lakini mgonjwa akichelewa kufika hospitalini huenda akabaki na tiba za kupunguza makali ya ugonjwa na kurefusha maisha pekee.
Jinsi ya kulinda afya ya ini
Dkt. Pazi amewataka wananchi kujikinga dhidi ya maambukizi ya homa ya ini kwa kufanya ngono salama na kuepuka matumizi ya vifaa vinavyoweza kuwa na damu ya mtu mwingine.
Chat Nasi Whatsapp
"Ungana na Wasomaji zaidi ya 12,000 wanaopata huduma ndani ya afyaclass,Kama unachangamoto yoyote ya kiafya;Kwa Ushauri&Tiba tuwasiliane hapa kupitia WhatSapp,Kama huna Whatsapp tuma SMS au Piga +255758286584."
Chat WhatSapp HapaPia amesisitiza umuhimu wa wanawake wajawazito kupima, kwa kuwa virusi vya homa ya ini B vinaweza kuambukizwa kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto wakati wa kujifungua.
Kupunguza au kuacha matumizi ya pombe na sigara pia kunaweza kusaidia kulinda ini dhidi ya madhara.
Fahamu Pia,Chanjo inapatikana kwa ajili ya kuzuia homa ya ini B, huku homa ya ini C ikiwa na dawa zinazoweza kuitibu.
Wananchi wahimizwa kwenda kupima,Wananchi wamehimizwa kupima na kufahamu afya ya ini, hata kama hawana dalili zozote.
“Kupima kunasaidia kugundua tatizo katika hatua za mwanzo. Ukijua afya yako, inakuwa rahisi kupata matibabu yanayofaa,” amesema Dkt. Pazi.
#Soma Ugonjwa wa Homa ya Ini Pamoja na Dalili Zake Hapa
References:
- UN_swahili-Fahamu Kuhusu Ugonjwa wa Homa ya Ini
- Ugonjwa wa Homa ya Ini Pamoja na Dalili Zake Hapa
Medical Disclaimer
Medical Disclaimer: Taarifa kwenye makala hii ni kwa ajili ya Updates au elimu ya jumla tu na haichukui nafasi ya uchunguzi,Tiba au ushauri wa kitaalamu wa daktari kwa mtu mmoja mmoja. Kama una dharura au tatizo lolote la kiafya, tafadhali Wasiliana na Daktari moja kwa moja hapa.
Je, unahitaji ushauri binafsi au matibabu ya tatizo lolote?
💬 Wasiliana na Daktari Hapa