Ticker

6/recent/ticker-posts

FAIDA ZA KUTOA MACHOZI-AFYA YA MACHO



AFYA YA MACHO

National Eye Institute (NEI) wanasema watu wanaolia mara kwa mara huwa na uwezo wa kuona vizuri na kuimarisha afya ya macho yao kuliko watu ambao hawalii mara kwa mara


SUMU NA VIJIDUDU VYA MAGONJWA

Machozi huwa na vimeng’enya (enzymes) za lysosome ambazo huvunjavunja na kuharibu sumu na vijidudu vya magonjwa mwilini ambavyo hutolewa nje kupitia machozi


HUTOA NJE HOMONI ZA STRESS

Binadamu anapolia kutokana na stress mbalimbali zinazomkabili maishani,machozi yake huwa na wingi wa homoni zinazosababisha hali hii.Kupitia kulia,homoni hizi hutoka nje ya mwili hivyo kumfanya apone majeraha ya moyo na nafsi mapema.Ndiyo maana wanawake husahau na kusamehe mapema zaidi kuliko wanaume.Wanalia sana


HUONGEZA FURAHA

Baada ya kulia,furaha hurejea.Kitendo cha kulia husisimua uzalishwaji wa homoni za oxytocin na endorphins (homoni za mapenzi na furaha) ambazo huongezeka sana kwenye mzunguko wa damu.Ndiyo maana mtu anapokuwa amekasirika sana kisha akalia,uwezo wa kuipata furaha ni mkubwa sana kuzidi yule aliyejifanya mbabe akazuia machozi yake yasitoke nje


HUONGEZA THAMANI

Pengine hii ndiyo silaha kubwa inayotumiwa na wanawake kuongeza ama kuteka hisia za wanaume.Hadi kufikia mwaka 2016,tafiti nyingi zilizokuwa zimefanyika zilithibitisha kuongezeka kwa hisia kutoka upande wa pili kwenda kwa mtu anayelia hasa jambo hili linapohusisha jinsia mbili tofauti.Japo hadi sasa hakuna maelezo ya kina kueleza uhusiano huu,bado sababu za msingi kabisa (kwa akili ya kawaida tu) zinathibitisha hili.Mfano,hakuna kitu kinachosumbua hisia za mwanamme kama kuona mke/mpenzi wake analia


Kulia siyo muhimu tu kwa afya zetu,ila ni muhimu pia katika harakati za maisha yetu ya kila siku


Cc #afyainfo

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!





Post a Comment

0 Comments