Ticker

6/recent/ticker-posts

FAIDA ZA KUTUMIA JUICE YA TANGO



  JE ZIPI NI FAIDA ZA KUTUMIA JUICE YA TANGO?

Aidha, tango linaaminika kupunguza kiwango cha mafuta mabaya mwilini (cholesterol), huimarisha misuli ya mwili na bila kusahau husaidia usagaji wa chakula tumboni hivyo kuondoa tatizo la ukosefu wa choo.

Virutubisho vilivyomo kwenye tango pia, hutoa afueni kwa mtu mwenye matatizo ya ini, kongosho, figo na matatizo katika kibofu cha mkojo.

Wataalamu wetu wanatueleza pia kuwa tango lina kirutubisho kinachojulikana kama ‘erepsin’ ambacho husaidia uzalishaji wa ‘amino acids’ ambazo ni muhimu kwa uzalishaji wa protini mwilini.

Vile vile, tango lina kiwango kingi cha Vitamin C, hivyo kuwa na uwezo mkubwa wa kuondoa matatizo yatokanayo na ukosefu wa Vitamin C, kama vile kutokwa na damu kwenye fizi, upungufu wa damu kwa watoto wachanga na kuota meno na mifupa vibaya.


KINGA YA SARATANI

Pengine faida kubwa kuliko zote unazoweza kuzipata kwa kula tango au juisi yake mara kwa mara ni kinga dhidi ya saratani za aina mbalimbali. Jambo hili linatokana na ukweli kwamba tango lina kiwango kikubwa cha ‘alkaline’ (uchachu). Kwa kawaida ‘seli’ za saratani ‘haziwezi kuishi’ kwemye mazingira yenye uchachu, hivyo tango kinga dhidi ya saratani.


DAWA YA MAGONJWA YA NGOZI

Tangu enzi na enzi, tango limekuwa likitumika katika masuala ya urembo wa ngozi, watu wengi hutumia tango kwa njia mbalimbali kutunza ngozi zao na kupendezesha sura zao. Hata baadhi ya vipodozi visivyo na madhara, hutengenezwa kutokana na tango.

Ulaji wa tango na unywaji wa juisi yake mara kwa mara, huondoa matatizo mengi ya ngozi yaliyomo ndani na nje ya mwili. Utakapotumia juisi ya tango kwa muda wa wiki mbili hadi tatu mfululizo, utakuwa na ngozi nyororo na yenye afya kushinda hata mtu anayetumia vipodozi.

CR: @afya_solution

karibuni Sana..!!





Post a Comment

0 Comments