Magonjwa
MADHARA YA VIDONGE VYA P2 KWA WADADA
![](https://afyaclass.com/mk_omb/uploads/2020/12/59262984_303.jpg)
MADHARA YA KUTUMIA P2
p2 ni dawa ya dharura (emergency contraceptive),inazuia mtu asipate Mimba kwenye mazingira ambayo umefanya sex pasipo kupanga na upo siku za hatari,au umelazimishwa kufanya sex au umebakwa,ili kuzuia mimba zisizotarajiwa unalazima Kunywa hizi dawa
Ni Dawa iliyotengenezwa kutumiwa mara chache tu,inapokulazimu.Sio dawa unayotakiwa kutumia kama njia ya uzazi wa mpango ya muda mrefu. Kuna wanawake humeza p2 kila mwezi,hii haitakiwi. Katika mazingira ya kawaida,haipaswi kumezwa zaidi ya mara 3 kwa mwaka. Kuendekeza kila mwezi kunywa hizi p2 sio sahihi,Unatakiwa ende hospitali ili upate njia sahihi ya uzazi wa mpango ya muda mrefu.
Baadhi ya Side effects/madhara ni ya matumizi holela ya dawa hizi ni
1.Unaweza kujisikia kichefuchefu au kutapika baada ya kumeza,
2.Maumivu ya tumbo
3.Matiti kuuma na kujaa
4.Pia hedhi zako zinazofuata zinaweza zikawahi au zikachelewa au zikatoka nyingi sana( ukiona zimezidi siku 8 fika muone daktari) au ukawa unapata hedhi nyepesi sana,au pia haupati hedhi kabisa (amenorhoea)
5.Kichwa kuuma na kizunguzungu
6.Mabadiliko ya Ute ukeni (change in cervical secretion,hapa unakuta Ute wa ovulation mtu hapati).
7.Kupata maambukizi ukeni,vaginal infections
8.Hatari ya kupata PID
9.Maumivu wakati wa sex(dyspareunia)
10.Mama anakuwa hatarini kutungisha mimba nje ya kizazi yaani ectopic pregnancy.
11.Lakini pia kuna wanawake hupata Ovarian cyst,vivimbe kwenye mfuko wa mayai.
Kuna sababu hapo juu kama PID,kutopata UTE,infections kwenye uke hizi zinakuja athiri mwanamke anakuwa anapata taabu kwenye Kupata mimba
Kama hujapanga kupata mimba,tafadhari fuata njia ya uzazi wa mpango ya muda mrefu inayokufaa,achana na kumeza p2 kila mwezi.
KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA JUU YA TATIZO LOLOTE TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.
-
Magonjwa5 days ago
Ugonjwa wa ngozi sehemu za siri
-
Uzazi/Ujauzito3 days ago
Dalili za hatari baada ya kujifungua kwa upasuaji
-
Elimu&Ushauri7 days ago
Afya za watu bilioni 1.8 duniani matatani kwa kutokufanya Mazoezi – WHO
-
Magonjwa2 days ago
Dalili za infection kwenye damu,mchafuko wa damu
-
Events4 days ago
Chad yafanikiwa kuondoa Ugonjwa wa trypanosomiasis,WHO yatangaza
-
Uzazi/Ujauzito13 hours ago
Dalili za mimba hutokea baada ya siku ngapi
-
News7 days ago
Mlipuko Mbaya wa homa ya nyani watokea tena KIVU KASKAZINI
-
News2 days ago
TANZIA:Yusuf Manji afariki dunia akipatiwa Matibabu Marekani