Ticker

6/recent/ticker-posts

TATIZO LA UKE MKAVU



  Kwa kawaida kwa kila mwanamke,uke wake unapaswa kuwa na hali ya unyevunyevu kutokana na ute mwepesi unaozalishwa ili kusaidia kuuweka uke katika hali hii.

Hormone inayojulikana kama estrogen ndo inayofanya kazi ya kufanya ute ute huu kuzalishwa ili kufanya uke kuwa na unyevunyevu na kuta za uke kuwa zinavutika(elastic).Pia ute huu husaidia kuweka sawa mazingira rafiki kwa mbegu za kiume,ili zinapokuwa  zimeingia zisiweze kufa hadi zinapolifikia yai.

Kushuka kwa kiwango cha hormone ya estrogeni ni chanzo kikubwa cha kupungua kwa ute huu na kufanya uke kuwa mkavu.Kiwango cha hormone kinaweza kushuka kutokana na sababu mbali mbali kama tutavyoona katika makala hii.

Inaweza kuonekana ni jambo dogo,lakini kutokua na unyevunyevu wa kutosha inaweza kuathiri maisha ya muhusika haswa katika swala la kujamiiana.Ikiwemo kusababisha tatizo la maumivu wakati wa tendo la ndoa, na kupata tatizo la fangasi za ukeni mara kwa mara

CHANZO CHA TATIZO
Tatizo la uke kuwa mkavu linawakumba sana watu waliofikia ukomo wa hedhi (Menopause) Kutokana na sababu kwamba mwanamke anapofikia kipindi hiki mwili unapunguza au kuacha kutengeneza hormone hii ya estrogen. Hali hii hupelekea kuta za uke kuwa nyembamba na hazivutiki tena hali ambayo kitaalamu inajulikana kama Vaginal Atrophy.

Kiwango cha estrogen kinaweza pia kushuka kutokana na vitu vifatavyo:

1.Kuzaa na kunyonyesha. Kipindi hiki mwili unazalisha hormone ya maziwa (prolactin hormone) ambayo pia inazuia kuzalishwa kwa hormone ya estrogen.
2.Matibabu ya saratani. (Tiba ya mionzi na dawa za saratani)
3.Kutolewa mifuko ya mayai( ovaries)
4.Dawa zinazozuia uzalishwaji wa hormone ya estrogen kwa watu wenye tatizo la Uvimbe kwenye kizazi, (fibroids na endometriosis)

SABABU NYINGINE ZA UKE KUWA MKAVU NI:
SJOGREN SYNDROME ,Huu ni ugonjwa ambao kinga ya mwili inaharibu cell zinazotengeneza huu unyevunyevu
Dawa kutibu mzio( allergy) na mafua
Kusafisha uke  hadi kwa ndani (douching)
Kusafisha uke kwa kutumia sabuni zenye kemikali
Kutoandaana kabla ya kufanya ngono.

Karibu Sana..!!




Post a Comment

0 Comments