Ticker

6/recent/ticker-posts

UGONJWA WA HOMA YA INI(HEPATITIS)



  UGONJWA WA HOMA YA INI(HEPATITIS)

Ugonjwa wa Homa ya Ini ni Ugonjwa unaoshambulia kiungo muhimu mwilini kinachojulikana kama INI, ambapo WANAWAKE wakiwa miongoni mwa kundi linaloshambuliwa sana na Ugonjwa huu. Ifahamike kwamba Ini linafanya kazi zaidi ya 500 katika miili yetu ikiwa ile ya kupambana na sumu yaani Untoxification,na kuchuja damu mwilini.

Zipo sababu mbali mbali ambazo huweza kufanya ini lisifanye kazi vizuri,au livimbe ambapo hii ndyo huitwa Hepatitis kitaalam,Mfano; Unywaji wa pombe kupita kiasi,maambukizi ya magonjwa, VIRUSI au uwepo wa sumu kwenye damu,vitu hivi vinaweza kuathiri utendaji kazi wa Ini.

MAKUNDI YA VIRUSI VINAVYOLETA HOMA YA INI (HEPATITIS)

Tafiti zinaonyesha kwamba,kwa AFRIKA,Maambukizi ya Homa ya Ini,ndiyo shida kubwa inayosumbua ini kuliko matatizo mengine kwenye Ini.

Kuna Aina Tano;
(1) HEPATITIS A

(2) HEPATITIS B✔️

(3) HEPATITIS C

(4) HEPATITIS D

(5) HEPATITIS E

Ambapo hepatitis B na C zikiongoza kwa kuwa sababu kuu za kusambaa ugonjwa wa homa ya ini na husambaaa kwa njia kuu ya Damu pamoja na majimaji yanayotoka mwilini mwa mgonjwa, mfano jasho,mate,mkojo,machozi,Mbegu za kiume n.k

Hepatitis B peke yake,inakadiriwa kuwa, husababisha vifo kwa Takiribani watu 600,000 hivi kwa kila mwaka kutokana na Takwimu za Vifo DUNIANI. Na zaidi ya watu billion mbili sawa na asilimia 33% ya watu wote Duniani wameshaambukizwa virusi hivi vya Homa ya ini (Hepatitis B)

VIRUSI HIVI HUSAMBAA KWA NJIA GANI (HEPATITIS B NAC)?

Chanzo kikubwa cha kusambaa kwa maambukizi haya ni kwa Njia ya Damu,au majimaji kutoka kwa mgonjwa mfano; jasho lake,mate,mkojo,machozi,mbegu za kiume n.k na Hatari ya virusi hivi ni kwamba vina nguvu ya kuathiri au kushambulia mtu mara 100 zaidi ya virusi vya Ugonjwa wa UKIMWI.

NJIA AMBAZO MTU ANAWEZA KUPATA VIRUSI HIVI

NB; Njia zote ambazo virusi vya ukimwi husambaa,ndyo njia hizo hizo virusi vya Homa ya Ini Husambaaa.

(1) Mama mwenye virusi hivi anaweza kuvisambaza kutoka kwake kwenda kwa mtoto wakati wa Kujifungua ambapo uwezekano ni mkubwa zaidi ya asilimia 90% kama kusipochukuliwa tahadhari thabiti

(2) Kushiriki tendo la Ndoa na Mtu mwenye virusi hivi vya Homa ya Ini

(3) Kushare vifaa vyenye ncha kali kama wembe,sindano,miswaki n.k

(4) Kuongezewa damu ya Mtu mwenye virusi vya Ugonjwa huu wa Homa ya Ini

MDA AMBAO VIRUSI VYA HOMA YA INI HUWEZA KUISHI VIKIWA NJE YA MWILI

Virusi vya Homa ya Ini vinauwezo wa kukaa Nje ya mwili hadi siku 7 na bado vikawa na uwezo wa kuangia kwa mtu na kumuambukiza ugonjwa huu.

KUNDI LA WATU AMBAO WAPO KATIKA HATARI YA KUPATA UGONJWA HUU

(1) Watu wanaofanya Ngono zembe na pia wanashiriki kitendo hiki na watu wengi

(2) Watoto wanaozaliwa na mama mwenye ugonjwa huu wa Homa ya Ini

(3) Watu wanaotumia madawa ya kulevyia hasa aina ya Sindano

(4) Watu wanaoshiriki mapenzi ya Jinsia moja hasa wanaume

(5) Mtu mwenye mpenzi au mke mwenye virusi hivi

(6) Wagonjwa wenye magonjwa ya vigo ambao wanapata huduma ya kusafisha damu au kitaalam Dialysis

(7) Watumishi wote wa Afya

DALILI ZA UGONJWA WA HOMA YA INI

✓ kukojoa mkojo wenye rangi kama ya COCACOLA

✓Kupata rangi ya manjano katika maeneo tofauti ya mwili kama macho,mikono au mwili mzima ngozi hubalika rangi na kuleta rangi ya manjano

✓Hali ya kichefuchefu,kutapika,mwili kuchoka sana, na kukosa hamu kabsa ya kula chakula

Kumbuka; Maambukizi ya Ugonjwa wa Homa ya Ini,huweza kuwa chanzo kikubwa cha kuleta Ugonjwa wa Saratani ya Ini.

Ni muhimu sana kupima kwa Ugonjwa huu ili kuwa salama zaidi, hasa kwa makundi hatarishi niliyoyataja hapo juu.

KWA USHAURI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KUPITIA NAMBA +255758286584

Karibu Sana..!!







Post a Comment

0 Comments