Ticker

6/recent/ticker-posts

DALILI ZA MAAMBUKIZI KATIKA MFUMO WA MKOJO(UTI)



UTI

• • • • • •

Dalili za maambukizi ya mfumo wa mkojo ni zipi?

Dalili hutofautiana kulingana na ukali wa maambukizi,umri na sehemu iliyoathiri..


Dalili zinazojitokeza mara nyingi pakiwa na maambukizi (UTI):


📍Uchungu au kuwashwa unapokojoa.


📍Kuhisi kukojoa mara nyingi.


📍Homa na uchovu .


📍Mkojo wenye harufu mbaya na si safi (cloudy).


Dalili zinazotokana na maambukizi ya kibofu


📍Maumivu katika upande wa chini wa tumbo.


📍Kukojoa mkojo kidogo , wenye maumivu na mara nyingi.


📍Dalili za homa kidogo. Bila maumivu ya mbavu.


📍Damu kwenye mkojo.


Dalili zinazotokana na maambukizi ya upande wa juu wa njia ya mkojo


📍Maumivu ya upande wa juu wa mgongo na mbavu.


📍Kuwa na homa na kuhisi kibaridi. Kichefuchefu, kutapika, uchovu na kujihisi mgonjwa kwa ujumla.


📍Kuchanganyikiwa kwa wazee.


Maambukizi haya ni hatari sana yasipotibiwa vyema na haraka. Aidha yanaweza hata kuhatarisha maisha.






Post a Comment

0 Comments