Ticker

6/recent/ticker-posts

SABABU ZINAZOCHANGIA TATIZO LA BAWASIRI



BAWASIRI

• • • • • •

Bawasiri ni ugonjwa katika njia ya haja kubwa, hujitokeza kama uvimbe au kijinyama ambacho huweza kuonekana hadi nje. Kwa kiingereza hujuliakana kama haemorrhoids au piles.


Bawasiri inaweza kupelekea upungufu wa damu mwilini. Bawasiri inaweza kutibika ama kwa upasuaji ama kwa matumizi ya dawa mbadala kwa kipindi kirefu wiki hata 6 au hata zaidi kutegemea ilikuwa imejijenga kiasi gani.

Bawasiri husababishwa na nini

Hakuna sababu ya moja kwa moja inayojulikana kisayansi kwamba ndiyo husababisha bawasiri, bali mambo yafuatayo yanaweza kupelekea wewe kupatwa na ugonjwa huu:


1. Kufunga choo au kupata choo kigumu kwa muda mrefu

2. Ujauzito – wakati wa ujauzito watu wengine wanaweza kupatwa na bawasiri sababu ya msukumo wa mtoto karibu na sehemu ya kutolea haja kubwa

3. Kushiriki mapenzi kinyume na maumbile

4. Uzee – kadri miaka inavyosogea ndivyo inavyokuwa rahisi kwako kupatwa na ugonjwa huu kwa baadhi ya watu

5. Sababu za kurithi – baadhi ya watu wanaweza kurithi udhaifu wa ukuta huo wa njia haja kubwa ingawa ni asilimia ndogo sana.

6. Kuharisha sana kwa muda mrefu

7. Kutumia vyoo vya kukaa

8. Kunyanyua vyuma vizito

9. Mfadhaiko/stress

10. Uzito na unene kupita kiasi nk

Dalili za bawasiri

1. Maumivu wakati wa kujisaidia haja kubwa

2. Damu kunuka kinyesi wakati wa kujisaidia

3. Muwasho sehemu ya tundu la haja kubwa

4. Uvimbe au kinyama kujitokeza sehemu ya tundu la haja kubwa

5. Haja kubwa yaweza kujitokea tu muda wowote

#afyadarasa #afyaclass

.


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!








Post a Comment

0 Comments