Ticker

6/recent/ticker-posts

UGONJWA WA PID KWA KINA NA WATU WALIOPO KWENYE HATARI YA KUPATA PID



UJUE UGONJWA WA PID KWA KINA NA WATU WALIOPO KWENYE HATARI YA KUPATA PID

• • • • • •

Ni ugonjwa unaoshambulia mfumo Wa uzazi Wa mwanamke hasa kwenye kizazi(uterus),mirija ya mayai(oviduct) na ovari na hata na maeneo jirani ambayo sio viuongo vya uzazi.. Kwa asilimia 99% ya watu wenye PID hua wanakuaga na magonjwa ya zinaa kama kisonono na klamidia kabla ya kupata PID.Wapo wanawake wengine(asilimia 1) hupata PID kutokana na kupata vimelea Wa njia ya haja kubwa na kuwaingiza ukeni na wasokua na usafi mzuri wakati Wa hedhi. Kumbuka ugonjwa huu unaweza kushambulia sehemu moja au ikashambulia vyote kwa wakati mmoja.Kumekua na wimbi kubwa la watu mitandaoni wanatumia PID kufanya biashara haramu na mwili Wa mwanamke..

Magonjwa ambayo ni chanzo cha PID ni KISONONO(99%),KLAMIDIA(99%),KISAMAKI(1%),JIPU LA UKE,TB YA UKE na MGEN(mdudu Mpya anaechipukia kwa kasi sana), WALIO KWENYE HATARI YA KUPATA PID

1) WANAOFANYA NGONO:Kufanya ngono pekee ni njia tosha ya kuambukizwa Magonjwa haya,wanawake ambao hawafanyi mapenzi kabisa hawawezi kupata PID..

2) KUA NA WAPENZI WENGI(MULTIPLE PARTNERS): Wanawake wenye wapenzi wengi kama kua na wapenzi wanne na kuendelea ndani ya kipindi cha miezi 6 wanakua na uwezekano Wa kupata PID Mara 20 zaidi ya wale wenye Mpenzi mmoja.

3) Kua na mwenza mwenye Magonjwa ya kuambukiza(STI in the partner): asilimia 30 ya wanaume wenye kisonono, klamidia,mgen hua hawana dalili,hata hivo ukikutana na yule anaaepata dalili basi uwezekano Wa kupata PID ni mkubwa.

4) UMRI(age): PID inawapata sana wanawake wenye umri Wa miaka 15 hadi 25, inawapata pia wanawake wenye umri zaidi ya miaka 35 lakini ni kwa asilimia ndogo sana.PID sio kuwapata wanawake ambao hawajavunja ungo(prepuberty) na ambao wamefikia ukomo Wa hedhi(post menopausal)

5) Kama ulishawahi kuumwa PID (Previous PID): kama ulishawahi kupata PID basi jua una uwezekano mkubwa Wa kujirudia na hasa kama mtu hatojilinda kwenye masuala ya mapenzi.

6) UZAZI WA MPANGO(Contraceptive method): njia ya uzazi Wa mpango ambazo zinamkinga mwanamke na PID ni kondomu na vidonge vya majira. Kitanzi kimeonekaka kuongeza uwezekano Wa kupata PID lakini na kwa ule mwez mmoja tu toka uwekewe.

7) Wanawake wenye kisamaki(bacteria vaginosis).

8) Wanawake wanaopiga deki uke. 

 #drngimi


.


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Karibu Sana..!!!







Post a Comment

0 Comments