Ticker

6/recent/ticker-posts

CHANZO CHA TATIZO LA MPASUKO WA MFEREJI WA HAJA KUBWA



MPASUKO

• • • • • •

CHANZO CHA TATIZO LA MPASUKO WA MFEREJI WA HAJA KUBWA


Tatizo hili huweza kumpata mtu wa umri wowote (mtoto,kijana na hata mzee), lakini pia tatizo la mpasuko wa mfereji wa haja kubwa huweza kutokea kwa mtu wa Jinsia yoyote yaani Mwanaume au mwanamke.


CHANZO CHA TATIZO LA MPASUKO WA MFEREJI WA HAJA KUBWA NI PAMOJA NA;


1. Mtu kushiriki mapenzi kinyume na maumbile


2. Kupatwa na tatizo la Choo kigumu ambalo huchukua mda mrefu


3. Kujisaidia kwa kujilazimisha na kwa kutumia nguvu nyingi


4. Mtu kuwa na shida ya kuharisha kwa mda mrefu


5. Kuwa na magonjwa mbali mbali ya zinaa ikiwemo ugonjwa wa kaswende


6. Kuwa na maambukizi ya virusi vya ukimwi


7. Kupatwa na shida ya saratani ya Njia ya haja kumbwa ambayo kwa kitaalam hujulikana kama Rectal Cancer


8. Kupatwa na magonjwa ambayo huhusisha miwasho mingi pamoja na kuvimba kwa eneo hili,ikiwemo pamoja na tatizo la kushambuliwa na Fangasi kwa muda mrefu


9. Kupatwa na ajali ambayo huweza kuhusisha kuchanika kwa maeneo haya


DALILI ZA TATIZO LA MPASUKO WA MFEREJI WA HAJA KUBWA NI PAMOJA NA;


- Mtu kuhisi maumivu makali wakati wa kujisaidia


- Kujisaidia kinyesi ambacho kimechanganyika na damu


- Nguo ya ndani kuwa na damu au matone tone ya damu baada ya kuivua



MATIBABU YA TATIZO LA MPASUKO WA MFEREJI WA HAJA KUBWA


✓ Matibabu ya tatizo hili hutegemea sana chanzo chake,mfano; kama tatizo limetokana na mgonjwa kushambuliwa na magonjwa mbali mbali basi atapewa dawa za kudhibiti magonjwa hayo, kama shida imetokana na kujisaidia choo kigumu basi mgonjwa atapewa dawa za kulainisha choo N.K



✓ Lakini kwa ujumla wake baadhi ya matibabu huhusisha matumizi ya;


 Zinc oxide ambazo ni Cream kwa ajili ya kupaka eneo la tatizo, Nitroglycerin, botox N.K


Lakini kama tatizo litakuwa kubwa zaidi basi njia salama kuliko zote ni Upasuaji.


MADHARA YA TATIZO HILI LA MPASUKO WA MFEREJI WA HAJA KUBWA NI PAMOJA NA;


- Mgonjwa kupatwa na maumivu makali wakati wa kujisaidia


- Mgonjwa kukosa amani  na furaha kabsa wakati akihisi haja kubwa


- Mgonjwa kupata maumivu makali wakati akishiriki tendo la ndoa


- Kutokwa na damu kwenye kinyesi


- Mgonjwa kuchafua Nguo ya ndani kwa damu au matone ya damu


- Mgonjwa kupata shida wakati wa kutembea




KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.







Post a Comment

0 Comments