Ticker

6/recent/ticker-posts

DALILI ZA UGONJWA WA UKIMWI KWENYE ULIMI NA MDOMO



 UKIMWI

• • • • • •

DALILI ZA UKIMWI KWENYE ULIMI NA MDOMO


UKIMWI Ni ugonjwa wa upungufu wa Kinga Mwilini yaani kwa kitaalam huitwa ACQUIRED IMMUNODEFICIENCY SYNDROME(AIDS) ambao husababishwa na Virusi(virusi vya ukimwi(VVU)) wanaojulikana kwa kitaalam kama HUMAN IMMUNODEFICIENCY VIRUS au kwa kifupi HIV. Mgonjwa mwenye maambukizi ya virusi vya ukimwi huweza kuonyesha dalili mbali mbali ila makala ya leo inagusia kuhusu dalili za ugonjwa wa ukimwi kwenye Ulimi.


DALILI ZA UGONJWA WA UKIMWI KWENYE ULIMI NA MDOMO NI PAMOJA NA; 


1. Mdomo wa mgonjwa wa ukimwi huweza kupata hali ya kukauka sana na kuwa mkavu mara kwa mara.


2. Kutokana na kukosekana kwa uzalishaji mzuri wa mate,meno ya mgonjwa wa ukimwi huweza kuwa katika hatari ya kuoza kwani mojawapo ya kazi ya mate ni pamoja na ulinzi wa meno.


3. Kupatwa na tatizo la kuwa na vidonda mdomoni,kwenye Ulimi na maeneo ya kuzunguka kwenye lips, Vidonda hivo huwa mithili ya Duara ambavyo huweza kutokea kwa nje au ndani ya mdomo pamoja na Ulimi.


4. Kushambuliwa na Fangasi wa Mdomoni mara kwa mara ambao kwa kitaalam hujulikana kama thrush au  Candidiasis.


5. Kupatwa na Vidonda vinavyoambatana na homa mara kwa mara, japo tatizo hili huweza kupotea kabsa baada ya mgonjwa kuwa kwemnye dawa za ARV's.



6. Mgonjwa kupatwa na tatizo la kuvimba Fizi za meno ambazo huambatana na maumivu hasa wakati wa kula kitu.


7. Ngozi ya fizi za meno kuwa na madoa doa yenye rangi kama ya Dhambarau.


8. Kuota vitu kama nywele au vikamba kamba kwenye Ulimi wa Mgonjwa.


9.Ngozi ya juu ya mdomo kuwa na mabaka mabaka ya rangi nyeupe.


Soma: Ugonjwa wa Ukimwi,chanzo,dalili na Tiba


KUMBUKA; Moja ya sehemu za kwanza kuonyesha dalili za Ugonjwa wa Ukimwi pamoja na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi ni pamoja na MDOMO NA ULIMI.

Hivo ukiona dalili hizi nenda hosiptal mapema kwa ajili ya Vipimo na uchunguzi zaidi.


NJIA AMBAZO MTU HUWEZA KUPATA MAAMBUKIZI YA UGONJWA WA UKIMWI NI PAMOJA NA;


- Kushare vifaa vyenye Ncha kali kama sindano na Nyembe


- Kupewa damu ya mtu mwenye maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi


- Kufanya Ngono zembe


- Kufanya mapenzi kinyume na maumbile


N.K


Soma: Ugonjwa wa Ukimwi,Chanzo,Dalili na Tiba


KWA USHAURI ZAIDI AU ELIMU TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.







Post a Comment

0 Comments