Ticker

6/recent/ticker-posts

DAWA YA FANGASI UKENI



 FANGASI UKENI

• • • • •

DAWA YA FANGASI UKENI


Zipo dawa nyingi ambazo hutumika katika matibabu ya Fangasi ukeni,huku zingine zikiwa za asili na zingine za hospital. Lakini kwa upande wangu nitaelezea baadhi ya dawa za hospital zinazotumika kutibu tatizo la Fangasi ukeni.


NB; Fangasi jamii ya Candida albicans ndiyo hushambulia sana sehemu za siri za mwanamke.


DALILI ZA FANGASI UKENI NI PAMOJA NA;


1. Mwanamke kupata miwasho sehemu za siri ikiwa ni pamoja na eneo la ngozi kati ya njia ya haja kubwa na sehemu za siri


2. Mwanamke kutokwa na uchafu wenye rangi kama maziwa,ambao huambatana na harufu mbaya ukeni


3. Sehemu za siri kuwa na michubuko pamoja na vidonda kwenye mashavu na ngozi ya ukeni


4. Ngozi ya sehemu za siri kubadilika rangi na kuwa nyekundu


5. Kupata maumivu wakati wa tendo la Ndoa


MADHARA YA FANGASI WA UKENI NI PAMOJA NA;


- Mwanamke kunuka au kutoa sehemu zake za siri


- Mwanamke kutokwa na uchafu mithili ya maziwa Mgando


- Mwanamke kuwa mkavu na Kupata maumivu wakati wa tendo la ndoa


- Sehemu za siri za mwanamke kuwa na michubuko pamoja na vidonda


- Kukosa raha ya tendo la Ndoa


- Kukerwa na miwasho sehemu za siri hata ukiwa mbele za watu


- Fangasi sugu huweza kukusababishia hata tatizo la kutokushika mimba



DAWA YA FANGASI UKENI


• Baadhi ya Dawa ambazo hutumika hospitalini kutibu fangasi wa ukeni ni Pamoja na Clotrimazole ambapo kuna Cream ya kupaka sehemu za siri pamoja na ile ya vidonge vya kudumbukiza ukeni,ambapo vinaweza kuwa vitatu au sita, Na mwanamke hudumbukiza kimoja kimoja kila akilala mpaka amalize dose.


Tazama kwenye picha hapa chini kuona mfano wa Clotrimazole Cream ya kupaka


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.