Kondomu kupanda Bei duniani kwa 30% kufuatia vita vya Marekani,Israeli na IranAfyaclass Forum •

Mtengenezaji mkubwa zaidi wa kondomu duniani, Karex Bhd, ametangaza mipango ya kuongeza bei kwa kati ya asilimia 20 na 30, akitoa mfano wa usumbufu unaoendelea wa mnyororo wa usambazaji unaohusishwa na mzozo wa Iran.

Mtendaji mkuu Goh Miah Kiat alisema kampuni hiyo inaweza kuongeza bei zaidi ikiwa usumbufu utaendelea, huku gharama zinazoongezeka za malighafi na vifaa zikiendelea kuzorotesha shughuli.

"Hali ni tete sana, bei ni ghali ... Hatuna chaguo ila kuhamisha gharama hivi sasa kwa wateja," alisema. Karex hutoa zaidi ya kondomu bilioni tano kila mwaka na hutoa chapa kuu kama vile Durex na Trojan, pamoja na mifumo ya afya ya umma ikiwa ni pamoja na Huduma ya Kitaifa ya Afya nchini Uingereza na programu za kimataifa zinazoendeshwa na Umoja wa Mataifa.

Kampuni hiyo pia inakabiliwa na ongezeko la mahitaji, huku matumizi yakiongezeka kwa takriban asilimia 30 mwaka huu. Goh alihusisha hili na kupungua kwa akiba ya kimataifa, iliyozidishwa na kupunguzwa kwa ufadhili wa misaada ya kigeni, haswa kutoka kwa Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani.

 Changamoto za mnyororo wa ugavi zimeongezeka tangu kuongezeka kwa mzozo wa Iran mwishoni mwa Februari, na kuathiri upatikanaji wa vifaa muhimu kama vile mpira wa sintetiki, nitrile, karatasi ya alumini na mafuta ya silikoni, vyote vikiwa muhimu kwa uzalishaji wa kondomu.

Ucheleweshaji wa usafirishaji umezidisha tatizo hilo, huku muda wa uwasilishaji katika masoko ya Ulaya na Marekani ukiongezeka kutoka takriban mwezi mmoja hadi karibu miezi miwili.

0 Comment

Italia haiwezi kuchukua Nafasi ya Iran kwenye kombe la DuniaAfyaclass Forum •

Italia haiwezi kuchukua Nafasi ya Iran kwenye kombe la Dunia

Vuta nikuvute katika kutafuta Nafasi kwenye Kombe la Dunia,Pendekezo la Italia kuchukua nafasi ya Iran kwenye Kombe la Dunia la mwaka 2026 lakataliwa,

Mjumbe mmoja wa Marekani anayefahamika kwa jina la Paolo Zampolli alitoa pendekezo kwamba Italia ipewe nafasi ya Iran kutokana na mzozo unaoendelea kati ya Iran, Marekani na Israel,

Hata hivo Shirikisho la Soka Duniani, FIFA limekataa Pendezo hilo,Waziri wa michezo wa Italia, Andrea Abodi na Waziri wa Uchumi, Giancarlo Giorgetti pia wamekataa pendekezo hilo wakisisitiza kwamba kama ni Italia kushiriki Kombe la Dunia lazima ishinde uwanjani na sio kwa njia za aina nyingine kama hii.

0 Comment

Madhara ya kuangalia picha chafu maarufu kama PornographAfyaclass Forum •

Madhara ya kuangalia picha chafu maarufu kama Pornograph

Watu wengi wameathiriwa sana na Utazamaji wa Picha chafu au Video chafu au Pornograph(X) au Video/Picha za Ngono,hali ambayo imewaingiza kwenye Uraibu au Addiction,Kiasi kwamba hata mahusiano halisi hawaridhishwi nayo(relationship satisfaction),
Wengine wameingia kwenye hatari ya kupata athari kubwa ya Ubongo,Matatizo ya afya ya akili ikiwemo;Swala la wasi wasi(Anxiety), huzuni(Depression) pamoja na Aibu ambayo hawajui inatokana na nini.
Hebu tuaangalie Baadhi ya Madhara unayoweza kupata kwa kutazama Video au Picha Chafu(Video au picha za ngono)

Madhara ya kuangalia picha chafu maarufu kama Pornograph

1.Mabadiliko kwenye Ubongo pamoja na Mfumo wa Neva kwa ujumla:

Kutazama video au Picha chafu(za ngono) kunaweza kufanya kazi kama uraibu wa dawa za kulevya, na kusababisha kutolewa kwa dopamini kupita kiasi ambayo huchochea mfumo wa Ubongo unaohusika na hisia,Hali inayoweza kusababisha kupotea kwa hisia. 
Uchunguzi unaonyesha kuwa inaweza kusababisha athari katika maeneo ya ubongo yanayodhibiti kufanya maamuzi na udhibiti wa msukumo.

2.Matatizo kwenye Mahusiano halisi(Relationship Issues): 

Kuangalia Pornograph mara nyingi husababisha kupungua kwa kuridhika kingono na mweza halisi, kupungua katika uhusiano, na kupungua kwa urafiki.
Kwahyo unaweza kuingia katika hali ya kutokuridhika kingono, hali ambayo huweza kuleta matatizo kwenye mahusiano.

3.Matatizo kwenye Afya ya Akili

Kama nilivyosema hapo awali, Ukishaingia kwenye Uraibu wa kuangalia Video au Picha Chafu(Video/Picha za Ngono),tayari upo kwenye athari za afya ya Akili, hapa utaanza kuona matokeo mbali mbali ikiwemo;
  • Kuwa na Wasi wasi Mkubwa(Anxiety)
  • Huzuni au Mfadhaiko(depression)
  • Hali ya kusikia Aibu
  • Au kujihisi na Hatia

4.Mabadiliko ya Kitabia: 

Tafiti mbali mbali huonyesha; Baadhi hukabiliwa na maudhui ya vurugu au ya kudhalilishwa kunahusishwa na kuongezeka kwa tabia za uchokozi kwa wanaume na kupungua kwa kujithamini/taswira mbaya ya mwili kwa wanawake. Inaweza kusababisha unyanyasaji wa kijinsia pia.

5.Matatizo ya nguvu za Kiume

Baadhi ya Tafiti huonyesha pia Kuangalia kupita kiasi Video au Picha za Ngono huhusishwa na hali ambayo hujulikana kama pornography-induced erectile dysfunction (PIED) kwa Wanaume.
Hali ambayo huathiri nguvu za kiume pamoja na uwezo wa Mwanaume Kushiriki tendo kwa Ufasaha Zaidi.

Bonus Point: Fahamu mambo ambayo hutokea kwenye Ubongo wako Ukiacha kuangalia Video au Picha Chafu(Video/Picha za ngono)

Ubongo wako hurudi katika hali yake ya kawaida ndani ya siku 90, Siku hizi 90 ndizo zinazohitajika kujisikia kama mtu tofauti kabisa. Urekebishaji wa vipokezi vya dopamine na ile raha ya kawaida na kuhisi kuridhika hurejea tena. Hamasa inarudi na nishati huelekezwa kwenye kazi ya mazoezi na malengo halisi ndani ya Ubongo.

Mvuto kwa watu halisi huongezeka zaidi ya Video au Picha Chafu(PORN).Umakini au Concentration huongezeka na kujiamini kunaongezeka zaidi.

Unyogovu,huzuni au Mfadhaiko(Depression) hufifia kadri aibu inavyopotea,Kujiamini na furaha ya asili inarudi. Hali ya Kupata Usingizi huanza kuimarika ikiwa ulikuwa hupati Usingizi n.k...

Acha Kuangalia Porn kwa afya ya Ubongo wako,afya ya uzazi na mwili wako kwa ujumla,ni Very addicted Kama Dawa za Kulevyia.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU NA TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Rejea Links Zilizotumika Pia;

  • https://pmc.ncbi.nlm.nih.gov/articles/PMC10399954/
  • https://culturereframed.org/adolescents-porn-and-mental-health-understanding-the-dangerous-effects-of-porn-on-developing-minds/#:~:text=It%20stimulates%20the%20release%20of,sexual%20problems%20in%20adult%20life
  • https://www.mentalhealth.com/blog/how-pornography-distorts-intimate-relationships#:~:text=Not%20all%20use%20is%20harmful,harm%20than%20the%20material%20itself.

0 Comment

Pambano la Anthony Joshua dhidi ya Tyson Fury litakuwa pambano kubwa zaidiAfyaclass Forum •

Pambano la Anthony Joshua dhidi ya Tyson Fury litakuwa pambano kubwa zaidi- bingwa wa zamani wa uzani wa juu David Haye atangaza.

Bingwa wa zamani wa uzito wa juu David Haye amesisitiza umuhimu wa pambano kati ya Anthony Joshua na Tyson Fury, akiliita pambano muhimu zaidi,

Uwepo wa pambano hilo ulichochewa zaidi mapema mwezi huu baada ya vigogo hao wawili kurushiana maneno katika Uwanja wa Tottenham Hotspur, Huku mashabiki zao wakihitaji Zaidi pambano hilo.

Akizungumza na Sky Sports, Haye alibainisha kuwa muda huo unaweza kuwanufaisha wapiganaji kifedha, akikiri, "Labda watapata pesa nyingi zaidi sasa kuliko wangepata wakati ulipozungumziwa kwa mara ya kwanza."

0 Comment

Rais Samia Suluhu Hassan afanya uteuzi na mabadiliko ya Viongozi mbali mbaliAfyaclass Forum •

Rais Samia Suluhu Hassan afanya uteuzi na mabadiliko ya Viongozi mbali mbali

Leo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi  kwenye nafasi mbali mbali Serikalini,

Moja ya Uteuzi uliofanyika ni wa Angela Charles Kizigha ambaye ameteuliwa kuwa Mshauri wa Rais, Masuala ya Jamii,

Pia Rais Samia suluhu amemteua Mobhare Holmes Matinyi kuwa Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika nchi ya Algeria. Mabadiliko hayo yamefanyika ndani ya Muda huu....

0 Comment

Mkunga aliyezalisha watoto zaidi 200 afariki dunia akijifungua Mtoto wake mwenyeweAfyaclass Forum •

Alikuwa mkunga aliyejitolea ambaye alitumia taaluma yake kusaidia kuleta watoto zaidi ya 200 duniani, mara nyingi akiwasaidia Wakinamama wengi kwa moyo wake wote. Akijulikana kwa uvumilivu wake na huruma na kujitolea kwa kina kwa huduma ya mama, alijenga uhusiano imara na familia zilizomwamini wakati wa baadhi ya nyakati muhimu zaidi za maisha yao. Kazi yake ilikuwa zaidi ya taaluma, ilikuwa wito uliojikita katika huduma na upendo.

Huyo mkunga anaitwa Janell Green Smith, na alikuwa raia wa Marekani (USA). Alifanya kazi Charleston, South Carolina. 

Kwa kusikitisha baada ya kujifungua mtoto wake mwenyewe, alifariki kutokana na matatizo yanayohusiana na kujifungua. Msiba huo umeitikisa sana jamii yake hasa wale waliomjua kama mtetezi wa akina mama na watoto wengi. Wengi wameelezea huzuni ya kupoteza mtu aliyejitolea maisha yake kuhakikisha uzazi salama lakini hakuweza kuishi maisha yake mwenyewe.

Kifo chake kimeibua mazungumzo kuhusu hatari za afya ya mama wakati wa kujifungua. Familia yake inapoomboleza na mtoto wake anakua bila uwepo wake, wengi wanaheshimu urithi wake kwa kutoa wito wa uelewa bora wa huduma na mabadiliko ya kimfumo.

0 Comment

Upendo Nkone akabidhiwa Gari Rasmi kutoka kwa Mashabiki ZakeAfyaclass Forum •

Upendo Nkone akabidhiwa Gari Rasmi kutoka kwa Mashabiki Zake

Ni Hafla iliyofanyika Aprili 23,Mlimani City jijini Dar es Salaam ambapo Msanii wa nyimbo za Injili Upendo Nkone alikabidhiwa Gari na Mashabiki Zake,

Kwa Furaha na Machozi,Upendo Nkone alitoa shukurani za Dhati na Kuwatamkia Baraka Wote waliotoa wazo hilo,na Wote Waliomchangia katika Changizo hilo,

Kwa kuthamini mchango wake mkubwa katika muziki wa injili na Huduma yake ya Uimbaji ambayo imebadilisha wengi,Mashabiki wa Upendo Nkone Waliamua Kumnunulia Gari.

Upendo Nkone aliwashukuru Kipekee Sana Resty Bulla pamoja na Lillian Mwasha ambao walisimamia Zoezi zima kwa Uwazi wa hali ya Juu ili kuhakikisha Zoezi hilo Linatimia.

Na Hatimaye Nkone akanunuliwa Gari na Wadau Mbali mbali ambao Walihusika katika Zoezi hilo.

Shukurani za Kipekee na Baraka Tele kutoka kwa Upendo Nkone aliziachilia kwa Kila aliyehusika kwa namna yoyote,ikiwemo kuchanga Pesa,Kutoa mawazo,au hata kuhudhuria tu kwenye hafla hiyo.

1 Comment
Notification
Karibu Afyaclass Forum Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Forum ASANTE.
UNDERSTOOD