Ticker

6/recent/ticker-posts

TATIZO LA KIUNGULIA KWA MAMA MJAMZITO



 KIUNGULIA KWA MAMA MJAMZITO

• • • • •

TATIZO LA KIUNGULIA KWA MAMA MJAMZITO


Moja ya tatizo ambalo humsumbua sana Mama mjamzito ni pamoja na kuwa na hali ya kiungulia cha mara kwa mara, hali hii humnyima au kumkosesha raha kabsa mama mjamzito.


CHANZO CHA TATIZO LA KIUNGULIA KWA MAMA MJAMZITO


- Sababu kubwa ya mama mjamzito kupatwa na Kiungulia ni kutokana na mabadiliko ya vichocheo vya mwili ambayo hutokea kipindi cha Ujauzito, na mabadiliko hayo huhusisha vichocheo mbali mbali kama Progesterone, Estrogen na Relaxin.


i). Hali hii ya mabadiliko ya vichocheo vya Progesterone  huhusisha uzalishaji wa kiwango kikubwa cha Progestrone,ambapo matokeo yake husababisha utembeaji wa chakula pamoja na kufyonzwa kwake kwenda taratibu sana.


ii). Uzalishaji wa kiwango kikubwa cha kichocheo aina ya Relaxin husababisha kulegea kwa misuli ya njia ya chakula, kutanuka kwa Njia ya chakula, pamoja na ring inayofungua na kufunga wakati chakula kinaingia tumboni kulegea, hivo kupelekea chakula kilichopo tumboni kurudi na kupanda juu, hapa ndipo mama mjamzito hupata kiungulia kikali kwani chakula pamoja na acid iliyopo tumboni hurudi na kupanda juu. 


MJAMZITO FANYA HAYA ILI KUPUNGUZA HALI YA KIUNGULIA


• Epuka tabia ya kula vyakula vingi kwa wakati mmoja


• Jitahidi kunywa maji mengi kwa siku nzima


• Epuka kula vyakula vyenye mafuta sana


• Epuka kula vyakula vyenye mchanganyiko wa viungo vingi


• Punguza ulaji wa vyakula vyenye kiwango kikubwa cha acid


• Jitahidi kuweka kitu kama mto wakati wa kulala na kuepuka kulala chini kabsa ili kupunguza uwezakano wa acid iliyopo tumboni kurudi na kupanda juu


• Epuka matumizi ya Sigara na Pombe kipindi cha Ujauzito, kwani mbali na madhara mengine ambayo huweza kumpata mtoto na mama,Pombe na sigara huweza kuchangia hali ya kiungulia


• Hakikisha huwi na tatizo la Uzito uliopita kiasi,hivo jitahidi kuweka sawa uzito wako wa mwili


• Epuka kuwa na Msongo wa mawazo au Stress nyingi wakati wa Ujauzito


• Epuka tabia ya kulala hapo hapo mara tu baada ya kula chakula


• Epuka kuvaa nguo zinazobana tumbo lako pamoja na kiuno chako


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.






Post a Comment

0 Comments