Ticker

6/recent/ticker-posts

TATIZO LA KUPATWA NA KIZUNGUZUNGU,CHANZO CHAKE NA MATIBABU YAKE



 KIZUNGUZUNGU

• • • • •

TATIZO LA KUPATWA NA KIZUNGUZUNGU,CHANZO CHAKE NA MATIBABU YAKE


Tatizo hili linawapata watu wengi, na wengine hata kufikia hatua ya kupata madhara mbali mbali kama kuanguka au kudondokea sehemu za hatari zaidi kama kwenye moto,Barabarani, N.K, hata kufikia hatua ya watu kupoteza kabsa maisha.


ZIPO SABABU MBALI MBALI ZA MTU KUPATWA NA HALI YA KIZUNGUZUNGU


Na miongoni mwa sababu hizo ni pamoja na;


1. Kuwa na tatizo la Shinikizo la Damu au kuwa na Ugonjwa wa Presha


2. Kuwa na tatizo la Magonjwa mbali mbali ya moyo,ikiwemo pamoja na tatizo la mishipa ya damu ndani ya moyo kuziba,moyo kuwa mkubwa N.K


3. Kuwa na matatizo ya Ugonjwa wa kisukari


4. Kuumwa Ugonjwa wa Malaria huweza pia kukusababishia hali ya kizunguzungu kikali


5. Kuwa na shida au matatizo mbali mbali yanayohusu masikio huweza kusababisha hali ya kizunguzungu kwa mhusika. Sehemu ya ndani kabsa ya sikio ina viungo ambavyo huhusika na kuleta hali ya usawa au BALANCE katika mwili,endapo pakitokea shida ndipo mtu hushindwa kubalance mwili wake na kuona hali ya kizunzungu.


6. Kuwa na shida ya Ongezeko la damu Kupita kiasi mwilini huweza kusababisha kizunguzungu kikali


7. Pia ifahamike kwamba matumizi ya baadhi ya dawa huweza kumsababishia mhusika kizunguzungu kikali


8. Kutokuwa na Mzunguko mzuri wa Damu katika mwili


9. Lakini pia damu kupungua sana mwilini huweza kusababisha hali ya kupepesuka na kizunguzungu kikali kwa mtu,wengine hata kuishiwa kabsa na nguvu na kudondoka chini


10. Pia endapo mtu kapata ajali ambayo imehusisha kugongwa Kichwa,au kuvuja Damu sana huweza kupata kizunguzungu kikali na hata kudondoka chini


MATIBABU AU VITU VYA KUFANYA KWA MTU MWENYE SHIDA YA KIZUNGUZUNGU.


- Kwanza kabsa matibabu ya Shida hii ya kizunguzungu yataanzia pale ambapo tumegundua chanzo chake ni nini. Lakini mgonjwa akifika hospital atafanyiwa vipimo mbali mbali kulingana na historia ya tatizo lake kama vile; vipimo vya wingi wa damu,Kipimo cha Presha, kipimo cha Sukari,Magonjwa ya moyo, kipimo cha Malaria N.K


Na ndipo chanzo cha tatizo huanza kutibiwa hapo hapo baada ya vipimo.


MADHARA YA KIZUNGUZUNGU NI PAMOJA NA;


• Kudondoka au kuanduka Chini


• Kuumia au kupata majeraha baada ya kudondoka


• Kupoteza Maisha



KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.







Post a Comment

0 Comments