Ticker

6/recent/ticker-posts

TATIZO LA MWANAMKE KUPATA HEDHI MARA MBILI KWA MWEZI



HEDHI

• • • • • •

TATIZO LA MWANAMKE KUPATA HEDHI MARA MBILI KWA MWEZI


Moja ya vitu ambavyo mwanamke hutakiwa kuvizingatia sana ni kuhusu mzunguko wake wa hedhi, Mzunguko wa hedhi huweza kumpa mwanamke kila aina ya ishara hata pale akiwa ni mgonjwa,kupitia mzunguko wa hedhi mwanamke anaweza kujua ana tatizo flani.


Mizunguko ya hedhi ipo tofauti kwa wanawake mbali mbali, Lakini kuna migawanyiko mikuu mitatu kwa kuangalia mda wa mzunguko wa hedhi yaani; 


(i) Kuna mzunguko wa hedhi mfupi mfano; siku 21


(ii) Kuna Mzunguko wa hedhi wa wastani au kawaida wa siku 28


(iii) Na kuna Mzunguko wa hedhi mrefu mfano; siku 35


Lakini kuna mizunguko ya aina mbili kwa kuangalia mabadiliko ya mzunguko wa hedhi yaani; 


(i) Kuna mzunguko usio badilika badilika au kwa kitaalam hujulikana kama REGULAR MENSTRUAL CYLCE


(ii) Na kuna mzunguko unaobadilika badilika yaani kwa kitaalam hujulikana kama IRREGULAR MENSTRUAL CYCLE


SABABU ZA MWANAMKE KUPATA HEDHI MARA MBILI AU ZAIDI NDANI YA MWEZI MMOJA NI PAMOJA NA;


1. Kuwa na tatizo la Mvurugiko wa vichocheo mwilini ambalo kwa kitaalam hujulikana kama Hormone imbalance.


2. Matumizi ya baadhi ya njia za uzazi wa mpango ambazo zina vichocheo kama progestrone na estrogen Mfano,Sindano,au vipandikizi(Vijiti).


3. Mwanamke kubadilisha mazingira au hali ya hewa,Mfano; kutoka sehemu moja ambayo amekaa kwa mda mrefu na kwenda sehemu nyingine ambayo hajawahi kukaa kabsa.


4. Mwanamke Kuwa na tatizo la uvimbe kwenye kizazi


5. Mwanamke kufanya kazi ngumu kupita kiasi


6. Pia mwanamke akifanya sana mazoezi ya mwili kupita kiasi huweza kupatwa na tatizo hili


Kuna baadhi ya wanawake hupata period mara mbili au zaidi kwa mwezi ambayo huambatana na maumivu makali sana ya tumbo hadi wengine kufikia hatua ya kulazwa kabsa hosptal.



KUMBUKA; Ukiona shida hii ni vizuri kukutana na wataalam wa afya ili kujua chanzo cha tatizo lako kwani hata magonjwa hatari kama uvimbe kwenye kizazi huweza kuwa na dalili kama hizi pia,hivo usipuuzie tatizo hili.



KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.





Post a Comment

0 Comments