Ticker

6/recent/ticker-posts

UKURUTU KWENYE MWILI,NGOZI,AU KWENYE KORODANI NA UKENI



 UKURUTU

• • • • •

UKURUTU KWENYE MWILI,NGOZI,AU KWENYE KORODANI NA UKENI


Tatizo hili la Ukurutu huweza kuwapata watu wa Jinsia zote(mwanaume&mwanamke) lakini pia na watu wa umri wowote ikiwemo watoto wadogo,vijana na hata wazee.


Ukurutu huu huweza kutokea maeneo mbali mbali katika mwili wa binadamu kama vile; ukurutu kwenye Ngozi ya mwili mzima au maeneo mbali mbali kama vile kwenye mikono,miguu,makalioni,mgongoni,shingoni,kwenye ngozi ya korodani za mwanaume, eneo la katikati ya sehemu ya haja kubwa ma sehemu za siri,au maeneo ya kwenye ngozi ya uke kwa wanawake.


CHANZO CHA TATIZO LA UKURUTU NI NINI?


Wataalam wa afya wanasema hakuna sababu ya moja kwa moja ya mtu kupatwa na tatizo hili la Ukurutu ila Zipo sababu mbali mbali ambazo huweza kuchangia mtu kuwa na shida hii ya ukurutu mwilini, na sababu hizo ni kama;


- Kuwa na allegery ya baadhi ya vitu, kama vile baadhi ya vyakula,Nyama, Sabuni,madawa au baadhi ya vitu vyenye kemikali ambazo una allergy nazo.


- Mabadiliko ya vichocheo mwilini, hii huhusishwa zaidi katika kipindi cha ujauzito ambapo baadhi ya wanawake wajawazito hupatwa na tatizo hili la ukurutu wa Ngozi na miwasho mwilini pindi wakiwa wajawazito.


- Mashambulizi ya vimelea mbali mbali vya magonjwa kama vile Virusi au Bacteria aina ya Staphlococcus aureus.


- Kusumbuliwa na tatizo la Fangasi, Wapo fangasi wanaoshambulia kwenye Ngozi na pia wapo fangasi wa kwenye Damu, Jamii hii ya fangasi wa kwenye Ngozi na kwenye Damu huweza kusababisha tatizo la Ukurutu na miwasho kwenye Ngozi.


- Mabadiliko ya hali ya hewa katika mazingira,Hapa tunazungumzia hali ya joto na jua kali pamoja na hali ya baridi kali,watafiti wanasema kuna baadhi ya watu hupatwa na hali ya ukurutu kwenye ngozi kipindi cha joto na jua kali,huku wengine wakipatwa na ukurutu kwenye ngozi kipindi cha baridi kali.


- Matumizi ya baadhi ya dawa au vipodozi vya Ngozi huweza kuleta reaction kwenye Ngozi na kusababisha tatizo hili la Ukurutu.


DALILI ZA TATIZO LA UKURUTU MWILINI


1. Kwa watoto wenye umri chini ya miaka miwili huanza kupatwa na upele kwenye Ngozi ya kichwani pamoja na mashavuni,huku upele huo ukiambatana na miwasho.


2. Kwa watoto wenye umri wa Zaidi ya miaka miwili hadi umri wa kubalehe,huanza kupata upele maeneo mbali mbali ya mwili kama vile kwenye miguu, magotini, shingoni au kwenye viganga vya mikomo.


3. Kwa watu wazima huanza kupata upele kwenye maeneo yote ya mikunjo,kama mikunjo ya magotini,viwiko vya mikono, maeneo ya ngozi ya shingoni N.K


4. Ngozi ya mwili kutoa vitu vyeupe mithili ya unga unaopukutika.


5. Kupatwa na miwasho kwenye Ngozi ya mwili hasa hasa maeneo yote ambayo yana upele upele.


NJIA MBALI MBALI ZA KUTIBU TATIZO HILI NI PAMOJA NA;


✓ Hakikisha unapaka mafuta vizuri Ngozi yako ya mwili ikiwemo maeneo yote yenye ukurutu


✓ Hakikisha hutumii vitu vyote ambavyo unaona vinakuletea hiyo allergy,kama chakula,sabuni,dawa,vipodozi vya ngozi N.K


✓ Epuka kuvaa Nguo za jamii ya mpira


✓ Hakikisha unapata matibabu sahihi ya Fangasi Kama una tatizo lolote la Fangasi Mfano; Fangasi wa kwenye Ngozi,Fangasi wa kwenye Damu N.K



KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.







Post a Comment

0 Comments