Ticker

6/recent/ticker-posts

AFYA KWA MAMA MJAMZITO(nukuu ya leo)



   MJAMZITO

• • • • •

AFYA KWA MAMA MJAMZITO(nukuu ya leo)


Kuna mambo mbali mbali ambayo yatamfanya mama mjamzito kufurahia maisha yake katika kipindi cha ujauzito. Na mambo hayo ni pamoja na;


1. Kuzingatia lishe bora kipindi cha ujauzito na mara baada ya kujifungua


2. Kujua dalili zote za hatari kipindi cha ujauzito kama vile; kutokwa na damu wakati wa ujauzito, mtoto kutokucheza tumboni kwa wale ambao wamefikia umri wa mtoto kucheza tumboni, kuvimba sana miguu,uso na mikono, Kutokwa na uchafu wenye harufu kali ukeni, Kushikwa na degedege,Joto la mwili kupanda au kuwa na homa N.K


3. Kutokuvaa nguo za kubana tumbo,mikanda N.K


4. Kutokuvaa viatu virefu wakati wa Ujauzito kwani huweza kukuletea madhara mbali mbali kama vile; Maumivu ya kiuno,mgongo,miguu kwenye visigino, kudondoka N.K


5. Pendelea kulala ubavu hasa hasa ubavu wa kushoto na sio kulala kifudifudi


6. Hakikisha unahudhuria kliniki zote 


7. Fanya maandalizi ya kujifungua mapema na jua vitu vyote ambavyo vinahitajika wakati wa kujifungua ambapo kwa kitaalam package hii hujulikana kama Individual birth preparedness(IBP)


8. Hakikisha unatumia vidonge vyekundu maarufu kama FEFOL au vidonge vya Folic acid, ambavyo hufanya kazi mbali mbali kama vile; kuongeza wingi wa damu kwa mama mjamzito kwani damu nyingi hupotea wakati wa kujifungua, kuzuia watoto kuzaliwa na mgongo wazi au tatizo la vichwa vikubwa.


9. Nenda hosptal pale unapohisi una tatizo lolote ambalo hulielewi wala usisubri siku ya kuhudhuria kliniki mfano; Tatizo la Chupa ya uzazi kupasuka N.K


10. Epuka matumizi ya dawa hovio pasipo maelekezo ya kina kutoka kwa wataalam wa afya, kwani dawa zingine huweza kukuletea madhara wewe pamoja na mtoto aliyetumboni.



-


KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.






Post a Comment

0 Comments