Ticker

6/recent/ticker-posts

FAIDA ZA KULA CHAKULA MUDA UNAOFANANA(kila siku)



  CHAKULA

• • • • •

FAIDA ZA KULA CHAKULA MUDA UNAOFANANA(kila siku)


Kwanza kabsa ifahamike kwamba, hata mwili nao huweza kujenga mazoea wenyewe kutokana na vitu ambavyo umeshazoeshwa kufanya kila siku, Mfano wewe ni shahidi kwamba,kama umezoea kulala usku muda flani, basi ukifika ule mda hata kama hutaki kulala kwa siku hyo utaona jinsi ambavyo utapata usingizi wa ajabu.


Au kama umezoea kukaa mazingira flani kwa muda mrefu basi ukiyabadilisha yale mazingira,tayari unaweza kupata mabadiliko flani kwenye mwili wako


Nidhahiri kwamba mwili hujenga mazoea kwa kitu flani ambacho unakifanya kila siku.


Hata katika Ulaji wa chakula mwili ni hivo hivo hujenga mazoea, na unaweza kupata madhara kama umebadilisha muda wa kula kila siku.


Kwanza unashauriwa kutokukaaa kwa muda mrefu sana bila kula chakula, Pili ukiwa unakula jaribu angalau kula chakula kwa muda unaoendana.


Kitendo cha kubadilisha badilisha muda wa kula chakula pamoja na kukaa kwa muda mrefu bila kula chakula huweza kusababisha kuwa na vidonda vya tumbo,


Kwani kinachotokea ni kwamba,Enzymes au vimeng'enyaji chakula pamoja na acid tumboni huanza kuzalishwa kwa ule muda ambao umezoea kula, hali ambayo hupelekea endapo tumbo litakuwa halina kitu, basi athari itaanza kutokea taratibu kwenye ukuta wa tumbo.


Kitu ambacho huweza kusababisha ukuta wa tumbo kulika na kuleta tatizo la vidonda vya tumbo.


ANGALIZO; Jitahidi kula kwa muda unaoendana au kufanana kila siku na epuka kukaa kwa muda mrefu bila kula chakula kwani unaweza kupata madhara mbali mbali kwenye mwili wako ikiwa ni pamoja na vidonda vya tumbo.



KWA USHAURI ZAIDI AU ELIMU TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.







Post a Comment

0 Comments