Ticker

6/recent/ticker-posts

MADHARA YA KUTUMIA DAWA YA FLAGYL(METRONIDAZOLE) PAMOJA NA POMBE(athari zake)



  FLAGYL

• • • • •

MADHARA YA KUTUMIA DAWA YA FLAGYL(METRONIDAZOLE) PAMOJA NA POMBE(athari zake)


Kwanza kabsa katika utangulizi wa makala hii,tuangalie matumizi mbali mbali ya dawa aina ya Flagyl au kwa jina lingine la kitaalam hujulikana kama Metronidazole


MATUMIZI YA FLAGYL PAMOJA NA KAZI ZAKE MWILINI


- Flagyl hutumika kutibu magonjwa au maambukizi yanayosababishwa na vimelea jamii ya parasite pamoja na bacteria mbali mbali kwenye mwili wako ikiwemo;


1. Maambukizi ya Giardia kwenye utumbo mdogo


2. Maambukizi ya amiba(amoeba) kwenye utumbo mkubwa


3. Maambukizi ya bacteria ambayo hujulikana kama Bacteria vaginosis, Trichomonas vaginal infections N.K


MADHARA YA KUCHANGANYA DAWA YA FLAGYL PAMOJA NA POMBE


Endapo upo kwenye dose ya flagyl(Metronidazole) huruhusiwi kutumia pombe kabsa,na endapo utachanganya vitu hivi viwili upo kwenye hatari ya kupatwa na madhara mbali mbali ikiwemo;


1. Kupatwa na shida ya viungo mbali mbali vya mwili kama figo pamoja na Ini


2. Kupatwa na tatizo la mapigo ya moyo kubadilika na kuanza kwenda mbio


3. Kupatwa na tatizo la kuishiwa pumzi na kushindwa kupumua kabsa,hali ambayo huweza kusababisha hata kupoteza maisha kabsa


4. Kupatwa na hali ya kuhisi kichefuchefu pamoja na kutapika


5. Kupatwa na kizunguzungu kikali hadi wengine kudondoka chini


6. Kupatwa na tatizo la maumivu makali ya kichwa


7. Joto la mwili kupanda gafla na kuhisi homa kali

N.K


Hivo basi ni hatari sana kuchanganya dawa ya Flagyl pamoja na pombe, epuka kabsa matumizi ya pombe ukiwa kwenye dose ya Flagyl kwani ni hatari kwa afya yako na maisha yako.



KWA USHAURI ZAIDI AU ELIMU TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.






Post a Comment

0 Comments