Ticker

6/recent/ticker-posts

TATIZO LA MAPIGO YA MOYO KUWA CHINI AU KUPUNGUA(maarufu kama bradycardia)



  BRADYCARDIA

• • • • •

TATIZO LA MAPIGO YA MOYO KUWA CHINI AU KUPUNGUA(maarufu kama bradycardia)


Katika hali ya kawaida endapo hakuna mabadiliko yoyote ndani ya moyo wako, hata moyo ukiendelea kudunda unaweza kusahau kabsa kama kuna moyo unadunda na kufanya kazi kila sekunde.


Lakini endapo kuna badiliko lolote mfano; mapigo ya moyo kuongezeka,moyo kwenda kasi sana au mapigo ya moyo kupungua sana,utaanza kuhisi mabadiliko makubwa kwenye mwili wako.


Katika makala hii tunazungumzia tatizo la mapigo ya moyo kupungua sana au kuwa kidogo,hali ambayo kwa kitaalam hujulikana kama bradycardia.


SABABU ZINAZOWEZA KUCHANGIA UWEPO WA TATIZO HILI LA BRADYCARDIA NI PAMOJA NA;


1. Misuli ya moyo kuchoka kufanya kazi kutokana na sababu ya kuzeeka au kuwa na  umri mkubwa


2. Kuharibika kwa tissu za moyo kutokana na hali ya uzee


3. Kuharibika kwa tissu za moyo kutokana na magonjwa mbali mbali ya moyo


4. Magonjwa ya moyo ambayo mtu huzaliwa nayo kwa kitaalam tunasema congenital heart diseases


5. Kuwa na tatizo la moyo kuvimba au kwa kitaalam tunaita myocarditis kutokana na maambukizi mbali mbali ya magonjwa


6. Kuwa na shida ya moyo kujaa maji


7. Kuwa na shida ya moyo kuwa mkubwa


8. Kuwa na tatizo la kuziba kwa mishipa ya moyo


10. Tatizo la tezi aina ya thyroid kufanya kazi chini ya kiwango yaani kwa kitaalam tunaita hypothyrodism


11. Kuwa na tatizo la moyo kufanya kazi chini ya kiwango kutokana na madhara ya operation iliyofanyika ya moyo


-

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.






Post a Comment

0 Comments